Msaada kwenye biashara ya nyanya

jojo joe

New Member
Joined
Sep 28, 2020
Posts
4
Reaction score
1
Habari wana Jf,

Nilikuwa nahitaji kufanya biashara ya nyanya ninunue kwa wakulima mashambani alafu nije kuuza kwenye masoko Dar.

Nilikuwa naomba.
1. Ushauri au muongozo kwa mwenye uzoefu na biashara hii inakuwaje na inafanywajwe.
2. Connection za wakulima wa zao hili.
3. Connection za masoko huku Dar hata sehemu nyingine zenye masoko ya uhakika.
 
Wewe upo wapi? Tuanze hapo
 
Nadhani Iringa, Morogoro ndo nyanya yakutupwa uko ukienda utakuta ndoo 2000 kwo kazi kwako
 
Mkuu mwaka huu nilienda tasaf ilula ni soko la nyanya kubwa ni biashara nzuri ila sokon ndo changamoto unaweza kukuta ilala lile box la nyanya limeuzwa 25000 alafu mabibo 28000 na wewe umepeleka ilala huku target yako ilikuwa bei ya 28000 inaelea manake kuna mtu anafunga hadi gari 3 kwenda sokon unakuta anapata hasara gari moja lingne linatoa hela
 
Biashara inaenda na madalali, tafuta dalali sokoni, njoo ilula chukua mzigo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…