Msaada kwenye hili tatizo.Mimi

Msaada kwenye hili tatizo.Mimi

The Donchop

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2014
Posts
294
Reaction score
378
Mimi ni mwanamke mwenye miaka 26 sasa. Toka nianze kupata period haijawahi kutokea nikakosa period on time. Ila this time imekuwa tofauti. Ni miezi miwili toka nisex na mwezi uliopita nilipata period kama kawaida lakini mwezi huu imegoma kabisa na sasa zimepita siku zaidi ya 15 na sina dalili yoyote ya kuingia period.
Nilipima mimba jana kwa kutumia pregnancy test na iliniletea matokeo negative.
Ninampango wa kwenda hospitali lakini nina hofu sana sababu ni mara ya kwanza kukutana na kitu kama hiki. Ni kheri ningekutwa positive nikajua ni mimba.
Naombeni mnisaidie wajuzi, angalau nipate pa kuanzia.
 
Ngoja wajuvi waje, ila inawezekana unatumia uzazi wa mpango au umebadilisha mazingira.
 
Tuliza akili yako kama ipo utapata tu na kama umepata mimba hormone zikiwa za kutosha pregnancy test itakuwa positive... Hofu yako inatoka wapi?
 
Ulikusudia kuwa na mimba au hukutaka kuwa nayo?

Aliyesex nawe anasemaje kuhusu hali hiyo?

PT iko sawa ila angalia tena baada ya muda mchache angalau wiki mbili huenda ukapata majibu zaidi

Ila ukiwa unakula uroda hukutuambia tungekushauri kitu labda
 
Tuliza akili yako kama ipo utapata tu na kama umepata mimba hormone zikiwa za kutosha pregnancy test itakuwa positive... Hofu yako inatoka wapi?
Hofu yangu nahisi pengine inaweza ikawa ni ugonjwa mkubwa
 
binti pole, usiwaze sana mabadiliko kwenu nijambo lisilokwepeka japo ikizidi sana pita hospitaliiiii! sawa mamah
 
nenda hospitali ukapime mimba afu urudi hapa kuleta mrejesho......

usisahau kuandaa mahitaji ya mtoto pindi atakapozaliwa.....

Goodluck....
 
May be una hofu,lakini pengine umebadilisha mazingira au hata vyakula. Tulia vuta week ahead pima tena. Wala si ugonjwa. Lakini ikizido sana basi onana na daktari.
 
Ulikusudia kuwa na mimba au hukutaka kuwa nayo?

Aliyesex nawe anasemaje kuhusu hali hiyo?

PT iko sawa ila angalia tena baada ya muda mchache angalau wiki mbili huenda ukapata majibu zaidi

Ila ukiwa unakula uroda hukutuambia tungekushauri kitu labda
Yeye sijamwambia bado. Sikuwa na dhamira ya kupata mimba.
 
Kwenye thread yako ile ya mwezi wa kwanza 2017 tarehe 30 uliandika una miaka 28 leo hii October 21/2017 una miaka 26....???
Mbona unatuchanganya hivi sasa au ni mimi sijaelewa inatoka 28 inaenda 26 au 26, 27 ndio 28....


Kuwa muwazi, saa nyingine umri pia unaweza kudetermine the way utakavyoshauriwa bibie
 
Hofu yangu nahisi pengine inaweza ikawa ni ugonjwa mkubwa
Ondoa shaka mambo ya kawaida tu kwa hedhi kubadilika kwa wanawake wala si ajabu. Kama ukibadili hali ya hewa na siku zinaweza kubadilika
 
Hivi kumbe huwa mnazimis period zenu. Binafsi huwa nawahurumia sana wanawake, mbona mbuzi wanapeta tu na hawana hayo makitu..

Na pia huwa natamani mgekuwa mnataga tu mayai tuwasaidie kuyakumbatia kuliko mnavyozaa..
 
punguza waswas sababu as long as unaongeza hofu ndio inavyozidi kukucheleweshea hedhi yako, je ulibadili mfumowowote wa lifestyle yako?? nikimanisha je umesafiri ndani ya mwezi uliomiss period yako?? kama umepima huna mimba then relax hutokea sometimes itakua normal tu
 
Back
Top Bottom