Jiandae uwe na pesa zaidi ya milioni moja, na inategemea eneo gani nyumba yako ipo kama una nguzo ipo tayari jirani na nyumba itakuwa rahisi kwako.Vile vile pale Tanesco kuna watu wanataka kupewa ahsante kabla ya kazi (inabidi utoe pesa sasa sijui rushwa au asante) Ukifanya vitu hivi utakuwa na umeme ndani ya 2 weeks.
Kama kuna mtu unamfahamu pale Tanesco pia inaweza kuchukua muda mfupi kufanikiwa kupata.
Bila kufanya vitu hivyo unaweza kuchukua hata mwaka hujapata umeme.
Mie sikufuuta 3 phase pale. Ningefuta hizo phase ningekutajia. Ila lile shirika la umeme lina usumbufu sana. Labda sasa watakuwa wamejirekebisha.
Muhimu mtafute fundi umeme anayefahamika pale Tanesco huyo anaweza kukurahisishia kazi.
U welcom.Thanks Pretty.
Asante sana hwa hizo heads up. Ubarikiwe!
nijulishe single phase ulivuta kwa bei gani...Jiandae uwe na pesa zaidi ya milioni moja, na inategemea eneo gani nyumba yako ipo kama una nguzo ipo tayari jirani na nyumba itakuwa rahisi kwako.Vile vile pale Tanesco kuna watu wanataka kupewa ahsante kabla ya kazi (inabidi utoe pesa sasa sijui rushwa au asante) Ukifanya vitu hivi utakuwa na umeme ndani ya 2 weeks.
Kama kuna mtu unamfahamu pale Tanesco pia inaweza kuchukua muda mfupi kufanikiwa kupata.
Bila kufanya vitu hivyo unaweza kuchukua hata mwaka hujapata umeme.
Mie sikufuuta 3 phase pale. Ningefuta hizo phase ningekutajia. Ila lile shirika la umeme lina usumbufu sana. Labda sasa watakuwa wamejirekebisha.
Muhimu mtafute fundi umeme anayefahamika pale Tanesco huyo anaweza kukurahisishia kazi.
Pretty anasema .......".Vile vile pale Tanesco kuna watu wanataka kupewa ahsante kabla ya kazi (inabidi utoe pesa sasa sijui rushwa au asante)....."
Halafu watu wa Tenesco wako hapa hapa na wanasoma,maana nilikuta wana internet connection 24/7,ninachojiuliza haziwasumbui statement za aina hii?Ningekuwa mimi ningekwisha hama kampuni hii kama siwezi kuibadili.
Kiboko yao nenda na recorder,wakikuomba hiyo pesa nenda na hiyo recorded voice kwa MD wao,utaupata in 7 days. Vishoka!vishoka!made in Tanesco-sisi ni ndugu zenu!
Mkuu hiyo ni culture tayari na siyo kwamba wakuu wao hawajui.
Mimi niliwahi kulipia umeme, pesa wakaila na risiti nilikuwa nayo.Tulisumbuana sana kwa karibia mwaka, hadi kupeleka ishu wizarani ikatoka amri umeme ukafungwa siku hiyohiyo! Nyie acheni tu!
Gharama za umeme kwa single phase na nguzo moja ni Tshs 1,374,000/=,bila nguzo haizidi TZS1million. Kwa nguzo mbili andaa pesa inayofikia TZS 2.5million na kwa nguzo tatu ama nne inabidi uwe na budget ya pesa isiyopungua 3 to 3.5 million.
Three phase hiyo ni balaa.kumbuka kuna VAT(ile 20% kodi ya nyongeza ya thamani) humo ndani ya hizo gharama kwa hivyo inapelekea gharama kuwa juu
Mkuu, nguzo tayari zipo nje ya nyumba. Kwa hiyo suala lipo kwenye kuconnect huo umeme.
Kama nguzo ipo nje ya nyumba, ni just Tsh 460,000 hivi!