Msaada: Mdogo wangu katumia mseto bila kujua kwamba ana mimba, sasa hivi analalamika tumbo linamuuma

Msaada: Mdogo wangu katumia mseto bila kujua kwamba ana mimba, sasa hivi analalamika tumbo linamuuma

Negrodemus

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2010
Posts
2,318
Reaction score
684
Wanajamvi naombeni msaada wenu mdogo wangu wa jinsia ya kike katumia dawa za mseto kumbe alikuwa na mimba ya wiki tatu yeye hajui sasa amekua akilalamika tumbo kwa zaidi ya wiki mbili sasa toka katumia dawa

Leo kaenda hospital kafanyiwa utra sound wanadai kuna bonge la damu kwenye kizazi je hilo bonge la damu ni mimba bado ipo au mimba imetoka na kama imetoka anasema hajableed kabisaa kuna dokta nimeongea nae anasema mpaka asafishwe sasa mimba ya miezi huwa inasafishwa.

Msaada wenu wadau mimba itakua bado ipo?

Pili kama imetoka mbona hajableed?

Tatu amekaa zaid ya wiki mbili atakuwa ameathirika au kudhurika?

Kuna dawa inaweza kutumika bila ya kisafisha kizazi? Kama ipo inaitwaje na gharama zake please..

Nawasilisha
 
Akisafishwa ndiyo hakuna mimba tena hapo. Itabidi asafishwe tu ingawa moja ya risk ni kuwa anaweza akachelewa sana kupata ujauzito mwingine. Mwambie siku nyingine akiuguwa malaria asitumie mseto inayouzwa 1,000/=
 
Mkuu,
Poleni sana kwa shida hiyo. Ukweli ni kwamba kiumbe hakina uzima tena ndiyo sababu daktari ameshauri asafishwe ili kutoa hicho kiumbe. Kama mwenyewe unavyosema ni zaidi ya wiki mbili kwa hiyo kuchelewa kumpeleka hospitali ili kusafishwa kunaweza kumletea madhara makubwa, kwani kiumbe kimeshapotea ila bado kipo mwilini. Ingekuwa amebleed, huenda kusingekuwa na haja sana ya kumsafisha, lakini inavyoelekea kutokana na maelezo yako ni kuwa mimba imeharibika lakini haijatoka. Kwa maana hiyo ni lazima asafishwe haraka ili mama awe salama. Akiwahi kupata huduma hiyo hatakuwa na madhara yoyote na ataweza kupata tena mtoto mwingine. Jipeni moyo, haya ni mambo ya kawaida na wakina mama wengi wameshayapitia, na baadaye wameweza kufanikiwa kupata watoto bila shida yoyote. Sababu za mimba kuharibika ni nyingi, lakini kama ulivyosema dada yako alitumia dawa za mseto za malaria. Cha kufanya ajitahidi sana asipate malaria wakati anapojiandaa kupata mtoto na pia wakati wote wa ujauzito wake. Ikitokea akapata malaria basi ahakikishe anatumia dawa chini ya uangalizi wa karibu wa daktari.
 
Asanteni sana kwa msaada wenu kesho ntampeleka hospital akapatiwe hiyo huduma.

Mungu awabariki
 
Back
Top Bottom