Msaada: Mgogoro wa aridhi mapiga bagamoyo

Msaada: Mgogoro wa aridhi mapiga bagamoyo

kidodosi

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2013
Posts
2,306
Reaction score
1,404

  • Mimi na jamaa zangu wawili, tumenunua Aridhi MAPINGA kijiji cha UDINDIVU wastani wa hekali moja kila mmoja kutoka Serikali ya kijiji,kila mmoja alilipa shilingi milioni tano{5,000,000} mwaka 2010.
    Mwaka 2013 mwenyekiti wa kijiji alitupa taarifa kwamba kuna mtu kajitokeza anadai yeye ni mmiliki wa hilo eneo kwahiyo shauri walilipeleka baraza la kata, Baraza likatoa maamuzi kwamba serikali ya kijiji ndiyo wamiliki wa eneo;

    Kutokana na maelezo ya mwenyekiti wa kijiji jamaa anayedai kwamba ni mmiliki alikata rufaa mahakani Kibaha na 2015 ameshinda kesi na amemilikishwa eneo.
    Kwahiyo basi mwenyekiti wa kijiji anasema kwa kuepusha usumbufu anatupatia eneo lingine.

    WASI WASI:
    1.Mpaka sasa hajanionesha nyaraka yoyote ya maamuzi ya baraza la kata wala Mahakama ya Kibaha.

    2.Sijawahi kukutanishwa na mtu anayedaiwa kuwa mmiliki wa hilo eneo.

    3.Eneo tulilouziwa kwa sasa limekatwa katwa viwanja na kupewa watu wengine, mwenyekiti wa kijiji anasema mmiliki amewagawia ndugu zae.


    Naomba ushauri :
    Nifanyeje ili kuhakikishiwa kwamba hilo eneo tunalopewa kama fidia halina mgogoro?
    ​



 
Wanajukwaa hii shauri naona mpaka sasa hamna aliye toa mchango wowote, hii inaonekana jinsi gani migogoro ya Aridhi inavyo sumbua jamii na serikali, nimeona shauri nililete hapa kwenye Jukwaa la Sheria.
msaada msaada msaada !!!!!!!!!!!!
 
Mwalimu Nyerere alikuwa na nia njema kabisa ya kutaifisha ardhi lakini cha kusikitisha ni kuwa hata watu waliokuwa karibu naye imewachukua miaka zaidi ya 25 baada ya kuachia madaraka kumwelewa alichokuwa anamaanisha. Na wamekuja kutambua hilo wakiwa tayari wameshaharibu, John Cheyo aliwahi kuuliza kuwa unaiita ardhi 'mali ya kijiji' wakati hao wajumbe wa serikali za vijiji wanaingia madarakani kwa rushwa na matokeo yake ni kuuza vijiji maana wao sio sehemu ya umiliki bali ni viongozi tu!
Hii itakusumbua, labda nawe uombe hukumu kama kweli ipo then ukakate rufaa mahakama ya juu kidogo japo ndio wale wale lakini waweza kubahatisha.
 
kidodosi hiyo ardhi uliinunua kwa nani?
Kuna taratibu za kununua ardhi kijijini. Wewe na aliyekuuzia mnaenda serikali ya kijiji, wanajadili maombi yako ya kutaka kununua ardhi, wakiridhika wanapeleka maamizi yao kwenye mkutano mkuu wa kijiji ili mamuzi yapitishwe au vinginevyo.

Vikao vyote viwili, yaani s/kijiji na mkutano mkuu wanaandika mihutasari ya maamuzi na nakala unabaki nayo.

Na unapotaka kununua ardhi ya kijiji ambacho wewe si mkazi unahitaji udhamini wa wanakijiji saba, wake kwa waume.

Mlifanya hivyo? Tuanzie hapo..
nipo barabarani nimeshindwa kuquote vifungu ila waweza kujisomea sheria ya ardhi ya kijiji namba 5 ya 1999 na kanuni zake ukipata.
 
Last edited by a moderator:
kidodosi hiyo ardhi uliinunua kwa nani?
Kuna taratibu za kununua ardhi kijijini. Wewe na aliyekuuzia mnaenda serikali ya kijiji, wanajadili maombi yako ya kutaka kununua ardhi, wakiridhika wanapeleka maamizi yao kwenye mkutano mkuu wa kijiji ili mamuzi yapitishwe au vinginevyo.

Vikao vyote viwili, yaani s/kijiji na mkutano mkuu wanaandika mihutasari ya maamuzi na nakala unabaki nayo.

Na unapotaka kununua ardhi ya kijiji ambacho wewe si mkazi unahitaji udhamini wa wanakijiji saba, wake kwa waume.

Mlifanya hivyo? Tuanzie hapo..
nipo barabarani nimeshindwa kuquote vifungu ila waweza kujisomea sheria ya ardhi ya kijiji namba 5 ya 1999 na kanuni zake ukipata.
Lusajo nashukuru sana ki ukweli hayo yote hatukufanya sisi tuli deal na mwenyekiti wa kijii na stakabadhi wakatupatia vile vile hatukuwa na mashaka maana kuna jamaa zetu walikuwa tayari wameuziwa na viongozi hao .
 
Mwenyekiti kakuibia


QUOTE=kidodosi;12524730]
  • Mimi na jamaa zangu wawili, tumenunua Aridhi MAPINGA kijiji cha UDINDIVU wastani wa hekali moja kila mmoja kutoka Serikali ya kijiji,kila mmoja alilipa shilingi milioni tano{5,000,000} mwaka 2010.
    Mwaka 2013 mwenyekiti wa kijiji alitupa taarifa kwamba kuna mtu kajitokeza anadai yeye ni mmiliki wa hilo eneo kwahiyo shauri walilipeleka baraza la kata, Baraza likatoa maamuzi kwamba serikali ya kijiji ndiyo wamiliki wa eneo;

    Kutokana na maelezo ya mwenyekiti wa kijiji jamaa anayedai kwamba ni mmiliki alikata rufaa mahakani Kibaha na 2015 ameshinda kesi na amemilikishwa eneo.
    Kwahiyo basi mwenyekiti wa kijiji anasema kwa kuepusha usumbufu anatupatia eneo lingine.

    WASI WASI:
    1.Mpaka sasa hajanionesha nyaraka yoyote ya maamuzi ya baraza la kata wala Mahakama ya Kibaha.

    2.Sijawahi kukutanishwa na mtu anayedaiwa kuwa mmiliki wa hilo eneo.

    3.Eneo tulilouziwa kwa sasa limekatwa katwa viwanja na kupewa watu wengine, mwenyekiti wa kijiji anasema mmiliki amewagawia ndugu zae.


    Naomba ushauri :
    Nifanyeje ili kuhakikishiwa kwamba hilo eneo tunalopewa kama fidia halina mgogoro?
    ​



[/QUOTE]
 
Back
Top Bottom