Msaada: Namna ya kufanikiwa kutunza fedha kwenye Kibubu

Msaada: Namna ya kufanikiwa kutunza fedha kwenye Kibubu

Sigara Kali

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2017
Posts
3,623
Reaction score
8,442
Salaam wana uchumi,wafanyabiashara na wajasiriamali.

Baada ya kuachana na akaunti ya bank miaka 6 iliyopita nlipokua natunza fedha zangu za boom na baada ya kumaliza chuo nkabaki choka mbaya akaunti ikafungwa

Kitaa napiga dili za hapa na pale sina hela ya kwenda kuitunza bank

Sasa Leo nimejikalia zangu ghetto nawaza na kuwazua mambo nkapata wazo nianze kutunza hela kidogo kidogo ninazopata kwa kutumia kibubu

Sasa wale wenye uzoefu wa kutumia kibubu ebu nipeni mbinu ya kufanikiwa kutunza fedha zangu ili siku nikivunja akaunti yangu ya kibubu nitoke na donge nono

Pia natakiwa niwe naweka hela kiasi gani kwa siku

Msaada please wa mawazo

Alamsiki.
 
" Tone moja moja la maji yadondokayo kutoka bombani hujaza ndoo".

Wazo lako ni zuri na unatakiwa uwe na nia pamoja na dhamira ya dhati kutimiza lengo lako.
Kuwa na kibubu ni jambo moja ila hicho utakachokuwa unakipata na kukiweka na kukitunza kunahitaji nidhamu ya pesa, hii inamaanisha lazima ujue kuiheshimu sarafu au pesa madafu unayotaka kudunduliza.
Mimi nilijaribu kutumia kibubu ila sikufanikiwa nilijikuta mara nyingi navunja kibubu kwa tamaa na mambo yasiyo na msingi na kushindwa kufokia malengo.

Baadae nikajifunza kuwa sikuwa na utayari wala dhamira ya dhati nikadhamiria kweli na badala ya kutumia kibubu nilisajili line ya mtandao fulani wa Simu nikawa naweka chochote na hatimaye nikatimiza lengo langu, line hiyo nilijiwekea lengo la kuweka pesa yoyote kwa miezi sita na kiukweli ilinisaidia sana sababu niliweka muda maalum na sikuwahi kushawishika kutoa pesa kabla ya wakati, ilikuwa inafika kipindi mambo tight ila nachakarika kupata mkwanja nje ya pesa ya kwenye line.

Kila la heri ,haba na haba hujaza kibubu.
 
Back
Top Bottom