Mwenzenu kuna kitu kinaniuma lakini sijui ni nini, leo ni weak ya pili sasa, yaani kifuani katikati ya mapafu nasikia kama kichomi flani hivi.
Sijawahi kupata tatizo hilo tangu nizaliwe. Sasa juzi nipo ofisini nimekaa gafla kikaanza, kilianza kwa kasi kilikuwa kimenikamata haswaa, ikabidi nilale, kilinikamata kama siku 2, baadae kikaacha kwa muda, lakini sasa kimerudia tena.
Ila sasa hakiumi sana, but nikibeba mzigo nakisikia, nikipiga hata chafya nakisikia, nikijinyoosha pia nakisikia. Naomba msaada ni kitu gani hiki???
Na je nifanyaje ??? Plz nisaidieni jamani sina raha