Mkuu hii biashara kwa sasa inaumiza sana kichwa kwani haya makampuni yanatoa commission ndogo sana!! Na hii biashara imekuwa kila uchochoro wakala, kwani kuna kipindi walikuwa wanatoa commission ya 10,000 kwenye transaction za milioni moja !!!!we huoni kuwa huu ni uhuni, nilimfungulia dogo nikaona ni zaidi ya wehu labda kama una biashara nyingine ndio uiingize humo hii biashara yaani isijitegemee yenyewe, na penyewe ni njia ya kutunza pesa yako tu.Ndio maana wengi wameshindwa .Kingine kuhusu hizo line siku hizi makampuni mengi hawatoi ukienda wanakwambia hamna ila ukimtafuta mfanyakazi personally anakuuzia kulingana na makubaliano yenu ila line za tigo ndio zina bei kubwa hazipungui laki 4, lakini airtel na voda hata kwa laki 150@ moja unaweza pata.Jaribu kufanya utafiti wa kutosha ndugu unaweza ingia gharama kubwa baada ya mwezi tu ukashindwa na kutafuta wa kumuuzia tena!! Labda kama huko kwenu mawakala bado ni wachache utaweza fanya miamala mingi sana kwa siku inaweza kuwa afadhari kidogo, kwani hapa mjini kila siku naona watu wanafunga hii biashara.