Msaada: Natibuje huu ugonjwa

Msaada: Natibuje huu ugonjwa

mischa

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
368
Reaction score
177
is


Huu ugonjwa wa ngozi umenisumbua sana umenipata mgongoni,nimetumia dawa za kila aina kwanzia fluconazole za kumeza hadi gentrisone za kupaka hauishii na bado unanirudia,je nautibuje wadau? au namuona mtaalam gani anisadie?
 
go and check for cancer treatment maana siku hizi ukiumwa sehem moja maranyingi itakuwa cancer check it mkuu..
 
Wataalamu wa magonjwa ya ngozi wanasema ni ugonjwa gani?
 
Kunywa na kupakaa mafuta ya ubuyu. Yanasaidia sana.
 
is


Huu ugonjwa wa ngozi umenisumbua sana umenipata mgongoni,nimetumia dawa za kila aina kwanzia fluconazole za kumeza hadi gentrisone za kupaka hauishii na bado unanirudia,je nautibuje wadau? au namuona mtaalam gani anisadie?

pole sana ndg mischa, nakushauri uende pale Manzese kwenye pharmarcy ya FABEK juu ghorani uliza daktari wa magonjwa ya ngozi huwa anapatikana hapo kila Jumatatu saa 10 jioni. Kama hutafanikiwa uje ulete mrejesho
 
aisee shukrani ntamtafuta na mrejesho ntauleta
 
pole sana ndg mischa, nakushauri uende pale Manzese kwenye pharmarcy ya FABEK juu ghorani uliza daktari wa magonjwa ya ngozi huwa anapatikana hapo kila Jumatatu saa 10 jioni. Kama hutafanikiwa uje ulete mrejesho

aisee ntaenda kumuona maana nasumbuliwa na huu ugonjwa
 
Mkuu.@mischa Ingelikuwa Bora uende Hospitali kupima na kujuwa una ugonjwa gani wa ngozi kuliko kutuonyesha hiyo tu picha haitosaidia kitu ili tuweze kukusaidia kukupa ushauri ni nini cha kufanya mimi nina hisi kwa uzoefu wangu utakuwa huo ugonjwa wako ni huu hapa chini unaitwa kwa jina MKANDA WA JESHI (HERPES ZOSTER/SHINGLES)



Ukanda%20wa%20jeshi.jpg

Kwa takribani miongo mitatu sasa, tumeshuhudia ongezeko kubwa la mlipuko wa ugonjwa wa mkanda wa jeshi linaloendana na ongezeko la hususani ugonjwa wa UKIMWI. Hali hii imefanya baadhi ya watu kuamini kuwa, ugonjwa huu ni dalili ya wazi kabisa ya mtu kuwa na VVU, imani ambayo kwa kiasi kikubwa ina ukweli ndani yake ingawa si kwa wote wanaopatwa nao.Mkanda wa jeshi au shingles au herpes zoster kwa

majina ya kitabibu ni ugonjwa unaosababishwa na virus wa aina ya Varicella-zoster ambao pia husababisha ugonjwa wa tetekuwanga au chickenpox. Ugonjwa huu huathiri ngozi ambapo huambatana na vipele na michubuko kama ya kuungua yenye kuambatana na maumivu makali
.
Visababishi
Kama tulivyokwisha tangulia kueleza hapo juu, ugonjwa huu husababishwa na virus aina ya Varicella-zoster ambao pia husababisha ugonjwa wa tetekuwanga. Baada ya mtu kupatwa na tetekuwanga, virus hawa hubaki katika hali ya kupooza/kutokuwa na madhara (dormant) katika neva

fulani za mwili. Baada ya miaka kadhaa, iwapo itatokea kinga ya mwili ikashuka kwa sababu yoyote ile, virus hawa hupata tena nguvu/kuwa na madhara (active), kuibuka na kusababisha ugonjwa wa mkanda wa jeshi.
Kwa kawaida shambulio la mkanda wa jeshi hutokea mara moja maishani ingawa laweza kujirudia.

Vihatarishi


Mkanda wa jeshi unaweza kumpata mtu wa umri wowote ule ingawa watu walio katika makundi haya wapo katika hatari kubwa zaidi:

• Wenye umri wa zaidi ya miaka 60
• Mtu aliyewahi kuugua ugonjwa wa tetekuwanga kabla ya umri wa mwaka mmoja
• Watu ambao kinga yao ya mwili imepungua kwa sababu mbalimbali kama vile matumizi ya aina fulan za dawa, magonjwa kama vile maambukizi ya VVU (HIV/AIDS), saratani na utapiamlo.

Je mkanda wa jeshi huambukizwa?

Hapana ugonjwa huu hauambukizwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine! Lakini iwapo itatokea mtoto au mtu mzima ambaye hajawahi kupatwa na ugonjwa wa tetekuwanga maishani mwake na ambaye pia hajawahi kupata chanjo dhidi ya ugonjwa huo akakutana na mtu mwenye ugonjwa wa mkanda wa jeshi, mtoto au mtu huyo atapatwa na ugonjwa tetekuwanga na siyo mkanda wa jeshi.
Ukanda%20wa%20jeshi%20picha.jpg


Dalili


Dalili ya awali kabisa ya mkanda wa jeshi ni maumivu makali sehemu fulani/ upande mmoja wa mwili yakiambatana na hali ya ganzi na hisia za kuungua kwenye ngozi. Maumivu pamoja na hisia za kuungua huwa makali sana na hutokea kabla ya vipele/michubuko kutokea kwenye ngozi.


Kawaida, vipele au michubuko huusisha eneo fulani la mwili kuanzia kwenye uti wa mgongo kuzunguka kuelekea eneo la tumbo au kifua. Michubuko pia inaweza kutokea kwenye maeneo yanayozunguka uso, macho, mdomo au masikio.
Dalili nyingine ni pamoja na :
• Maumivu ya tumbo
• Homa
• Maumivu ya mwili mzima
• Vidonda sehemu za siri
• Maumivu ya kichwa
• Maumivu ya viungo
• Kuvimba kwa mitoki/ matezi

Iwapo neva za maeneo ya uso zitaathiriwa, mgonjwa anaweza kupatwa na matatizo ya kuona, kuonja, au kusikia.

Vipimo


Ni nadra sana kufanya Vipimo maalum kwa ajili ya utambuzi wa ugonjwa huu, isipokuwa kwa nchi zilizoendelea. Kwa ujumla utambuzi wa ugonjwa huu hufanyika kwa kuchukua historia ya mgonjwa na kuchunguza sehemu ya ngozi iliyoathiriwa.

Vipimo vya damu yaani FBP huonesha ongezeko la chembe nyeupe za damu na antibodies dhidi ya virus wa tetekuwanga.

Matibabu


Matibabu ya mkanda wa jeshi hujumuisha matumizi ya dawa kama vile Acyclovir, Famciclovir na Valacyclovir kwa ajili ya kuua virus wanaosababisha ugonwja huu. Dawa hizi husaidia kupunguza maumivu, kuzuia madhara zaidi ya ugonjwa huu na kupunguza muda wa ugonjwa.


Dawa hizi hutolewa angalau saa 72 baada ya mgonjwa kuanza kuhisi maumivu na hali ya kuungua. Ni vema dawa zianze kutumika kabla ya vipele/michubuko kujitokeza.

Jamii ya dawa za corticosteroids kama vile prednisolone husaidia kupunguza maumivu na uvimbe kwa badhi ya wagonjwa. Dawa nyingine zinazofaa kutumika ni pamoja na jamii ya antihistamines kwa ajili ya kupunguza muwasho, dawa za maumivu, calamine lotion kwa ajili ya kupunguza muwasho. Aidha mgonjwa anashauriwa kupata mapumziko ya kutosha
Herpes%20zoster%20mgongoni.jpg


Matarajio

Mkanda wa jeshi kwa kawaida huchukua kati ya wiki mbili hadi tatu kupona wenyewe. Aidha ni nadra sana kwa ugonjwa huu kujirudia tena. Iwapo neva zinazothibiti mwendo katika mwili zitakuwa zimeathirika, mgonjwa anaweza kupatwa na kupooza kwa muda au kwa kudumu kwa sehemu ya mwili iliyoathiriwa. Wakati mwingine, maumivu yanayosababishwa na mkanda wa jeshi yanaweza kudumu kwa miezi mpaka mwaka hata baada ya mgonjwa kupona kabisa. Maumivu haya yanayojulikana kama postherpetic neuralgia kwa kawaida huwakumba wagonjwa wenye umri wa zaidi ya miaka 60 na husababishwa na uharibifu katika neva za mwili.

Madhara

Madhara ya mkanda wa jeshi ni pamoja na kupatwa na shambulio jingine la ugonjwa huu, maambukizi ya bakteria, upofu iwapo eneo la jicho litahusika, ukiziwi, maambukizi katika utando wa ubongo (encephalitis), uwepo wa vimelea kwenye damu (sepsis) au ugonjwa unaoitwa Ramsay Hunt Syndrome iwapo utahusisha neva za uso.

Kinga

Epuka kabisa kugusa eneo lenye vipele au michubuko kwa mtu mwenye mkanda wa jeshi au tetekuwanga iwapo hujawahi kuugua au kupata chanjo ya tetekuwanga.
Ni vema kupata chanjo dhidi ya virus wa Varicella zoster kama inapatikana katika nchi au eneo ulilopo . Tafiti zimeonesha kuwa, watu wazima wanaopata chanjo hii wana uwezekano mdogo sana wa kupata madhara ya mkanda wa jeshi kuliko wale wasiochanjwa.
Mkanda wa Jeshi (Herpes Zoster/Shingles)
 
is


Huu ugonjwa wa ngozi umenisumbua sana umenipata mgongoni,nimetumia dawa za kila aina kwanzia fluconazole za kumeza hadi gentrisone za kupaka hauishii na bado unanirudia,je nautibuje wadau? au namuona mtaalam gani anisadie?

naomba useme unaumwaje umwaje ili nijue ni ugonjwa gani na utumie dawa gani.
 
Mkuu.@mischa Ingelikuwa Bora uende Hospitali kupima na kujuwa una ugonjwa gani wa ngozi kuliko kutuonyesha hiyo tu picha haitosaidia kitu ili tuweze kukusaidia kukupa ushauri ni nini cha kufanya mimi nina hisi kwa uzoefu wangu utakuwa huo ugonjwa wako ni huu hapa chini unaitwa kwa jina MKANDA WA JESHI (HERPES ZOSTER/SHINGLES)



Ukanda%20wa%20jeshi.jpg

Kwa takribani miongo mitatu sasa, tumeshuhudia ongezeko kubwa la mlipuko wa ugonjwa wa mkanda wa jeshi linaloendana na ongezeko la hususani ugonjwa wa UKIMWI. Hali hii imefanya baadhi ya watu kuamini kuwa, ugonjwa huu ni dalili ya wazi kabisa ya mtu kuwa na VVU, imani ambayo kwa kiasi kikubwa ina ukweli ndani yake ingawa si kwa wote wanaopatwa nao.Mkanda wa jeshi au shingles au herpes zoster kwa

majina ya kitabibu ni ugonjwa unaosababishwa na virus wa aina ya Varicella-zoster ambao pia husababisha ugonjwa wa tetekuwanga au chickenpox. Ugonjwa huu huathiri ngozi ambapo huambatana na vipele na michubuko kama ya kuungua yenye kuambatana na maumivu makali
.
Visababishi
Kama tulivyokwisha tangulia kueleza hapo juu, ugonjwa huu husababishwa na virus aina ya Varicella-zoster ambao pia husababisha ugonjwa wa tetekuwanga. Baada ya mtu kupatwa na tetekuwanga, virus hawa hubaki katika hali ya kupooza/kutokuwa na madhara (dormant) katika neva

fulani za mwili. Baada ya miaka kadhaa, iwapo itatokea kinga ya mwili ikashuka kwa sababu yoyote ile, virus hawa hupata tena nguvu/kuwa na madhara (active), kuibuka na kusababisha ugonjwa wa mkanda wa jeshi.
Kwa kawaida shambulio la mkanda wa jeshi hutokea mara moja maishani ingawa laweza kujirudia.

Vihatarishi


Mkanda wa jeshi unaweza kumpata mtu wa umri wowote ule ingawa watu walio katika makundi haya wapo katika hatari kubwa zaidi:

• Wenye umri wa zaidi ya miaka 60
• Mtu aliyewahi kuugua ugonjwa wa tetekuwanga kabla ya umri wa mwaka mmoja
• Watu ambao kinga yao ya mwili imepungua kwa sababu mbalimbali kama vile matumizi ya aina fulan za dawa, magonjwa kama vile maambukizi ya VVU (HIV/AIDS), saratani na utapiamlo.

Je mkanda wa jeshi huambukizwa?

Hapana ugonjwa huu hauambukizwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine! Lakini iwapo itatokea mtoto au mtu mzima ambaye hajawahi kupatwa na ugonjwa wa tetekuwanga maishani mwake na ambaye pia hajawahi kupata chanjo dhidi ya ugonjwa huo akakutana na mtu mwenye ugonjwa wa mkanda wa jeshi, mtoto au mtu huyo atapatwa na ugonjwa tetekuwanga na siyo mkanda wa jeshi.
Ukanda%20wa%20jeshi%20picha.jpg


Dalili


Dalili ya awali kabisa ya mkanda wa jeshi ni maumivu makali sehemu fulani/ upande mmoja wa mwili yakiambatana na hali ya ganzi na hisia za kuungua kwenye ngozi. Maumivu pamoja na hisia za kuungua huwa makali sana na hutokea kabla ya vipele/michubuko kutokea kwenye ngozi.


Kawaida, vipele au michubuko huusisha eneo fulani la mwili kuanzia kwenye uti wa mgongo kuzunguka kuelekea eneo la tumbo au kifua. Michubuko pia inaweza kutokea kwenye maeneo yanayozunguka uso, macho, mdomo au masikio.
Dalili nyingine ni pamoja na :
• Maumivu ya tumbo
• Homa
• Maumivu ya mwili mzima
• Vidonda sehemu za siri
• Maumivu ya kichwa
• Maumivu ya viungo
• Kuvimba kwa mitoki/ matezi

Iwapo neva za maeneo ya uso zitaathiriwa, mgonjwa anaweza kupatwa na matatizo ya kuona, kuonja, au kusikia.

Vipimo


Ni nadra sana kufanya Vipimo maalum kwa ajili ya utambuzi wa ugonjwa huu, isipokuwa kwa nchi zilizoendelea. Kwa ujumla utambuzi wa ugonjwa huu hufanyika kwa kuchukua historia ya mgonjwa na kuchunguza sehemu ya ngozi iliyoathiriwa.

Vipimo vya damu yaani FBP huonesha ongezeko la chembe nyeupe za damu na antibodies dhidi ya virus wa tetekuwanga.

Matibabu


Matibabu ya mkanda wa jeshi hujumuisha matumizi ya dawa kama vile Acyclovir, Famciclovir na Valacyclovir kwa ajili ya kuua virus wanaosababisha ugonwja huu.
Nimeipenda hii ya kumshauri aende hospital, ningekuwa natumia pc ningekupa like.
 
niliambiwa unaitwa eczema
hiyo picha ni kama psoarisis,ila kama ni eczema, unasababishwa na allergy,na cha muhimu uangalie vyakula unavyokula,ni vizuri ukafanyiwa allergy test,kujua kitu gani kinakudhuru.vile vile ni vizuri uvae nguo za aina ya cotton,na sabuni za kuogea utumie zisizo na ma chemical.ukifata masharti huwa inasaidia.maana ugonjwa huo,unaweza ukajiona umepona,baadae ngozi inaharibika tena,ila kuna mafuta fulani yanaitwa lookman hayat tel,jaribu kuyatafuta maduka ya wahindi maybe na maduka ya waarabu ni mazuri mno,google utayaona yalivyo.
 
hiyo picha ni kama psoarisis,ila kama ni eczema, unasababishwa na allergy,na cha muhimu uangalie vyakula unavyokula,ni vizuri ukafanyiwa allergy test,kujua kitu gani kinakudhuru.vile vile ni vizuri uvae nguo za aina ya cotton,na sabuni za kuogea utumie zisizo na ma chemical.ukifata masharti huwa inasaidia.maana ugonjwa huo,unaweza ukajiona umepona,baadae ngozi inaharibika tena,ila kuna mafuta fulani yanaitwa lookman hayat tel,jaribu kuyatafuta maduka ya wahindi maybe na maduka ya waarabu ni mazuri mno,google utayaona yalivyo.
nashukuru ntayatafuta haya mafuta cjui hapa dar naweza yapata wapi?
 
nashukuru ntayatafuta haya mafuta cjui hapa dar naweza yapata wapi?
jaribu maduka ya wahindi yoyote yale. au hata maduka ya madawa,maana hiyo dawa ni from india inasaidia sana
 
Back
Top Bottom