Andresen
Member
- Feb 21, 2019
- 50
- 105
Ndugu zangu,
Ng'ombe wangu amezaa mwezi December, 2018. Lakini toka amezaa hali yake imekuwa sio kabisa. Anakula sana tena sana lakini anazidi kukonda kila siku na sasa amebaki mifupa tu na hali inazidi kuwa mbaya kwake.....ANGALIA PICHA YAKE HAPA CHINI.
Pia alipozaa mtoto mwezi December nilimwita mtaalamu alimchoma sindano, na baada ya mwezi alirudia kumchoma tena sindano akidai sasa atakuwa na afya nzuri lakini hali ndio imekuwa hivyo.
Kuna watu wameniambia huenda atakuwa na ugonjwa wa konokono wa kwenye maini, je inaweza kuwa ni kweli? Na kama ni kweli, je wataalamu wa mifugo mnashauri nitumie dawa gani ili kuweza kumnusuru huyu ng'ombe wangu?
Naombeni msaada wenu wa dawa sahihi kulingana na uzoefu na utaalamu wenu. Angalia picha yake hii hapa
Ng'ombe wangu amezaa mwezi December, 2018. Lakini toka amezaa hali yake imekuwa sio kabisa. Anakula sana tena sana lakini anazidi kukonda kila siku na sasa amebaki mifupa tu na hali inazidi kuwa mbaya kwake.....ANGALIA PICHA YAKE HAPA CHINI.
Pia alipozaa mtoto mwezi December nilimwita mtaalamu alimchoma sindano, na baada ya mwezi alirudia kumchoma tena sindano akidai sasa atakuwa na afya nzuri lakini hali ndio imekuwa hivyo.
Kuna watu wameniambia huenda atakuwa na ugonjwa wa konokono wa kwenye maini, je inaweza kuwa ni kweli? Na kama ni kweli, je wataalamu wa mifugo mnashauri nitumie dawa gani ili kuweza kumnusuru huyu ng'ombe wangu?
Naombeni msaada wenu wa dawa sahihi kulingana na uzoefu na utaalamu wenu. Angalia picha yake hii hapa