Msaada: Ni mtandao gani kwa sasa una bando nzuri za kushushia movie

Saidama

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2022
Posts
598
Reaction score
1,151
Kipindi cha nyuma kidogo Halotel walikua na bando ya gb10 kuanzia saa sita usiku hadi saa kumi na mbili alfajiri. Na sio Halotel tu, hata mitandao mingine ilikua na bando za usiku pia ambazo zilikua spesho sana kwa kushushia mizigo mikubwa kama movies na files nyingine zenye size kubwa. Kwa sasa ni kama hamna mtandao wenye bando ya usiku.

Kwa wazee wa kushusha movies, mnatumia bando ipi na ya mtandao gani kwa sasa kushushia movies?
 
Sahivi tunaangalia TBC tu..😂

Hivi mnaopakua movie huwa mnatafuta nini kwanini usiende tu kwenye site ukaangalia ikaisha!!.
Msije kuanza kuniita Freemason..😂
 
Serikali iliingilia kwa kuwapangia bei, na hii ilitokana na lawama za wananchi
 
Utangoja sana mpaka kukutana na mtandao kama huo
 
Kwa sasa mkombozi wangu ni TTCL.... Hawana ofa ya maana ila tofauti yake ni kwamba data zao zinalika kihalali.... Mfano nikiwa na GB 3 naweza kushusha muvi ya GB2.5 ikamalizika bila shida yoyote na zikabakia angalau MB300, hizo MB200 zinaweza potea kama slippage...

Mitandao mingine mfano Voda nikiwa na GB3 naweza download GB1.5 tuu kisha bando linakata... Ukijiuliza hizi GB1.5 zingine zimepotelea wapi huwezi kuelewa...

TTCL wana ofa yao moja ya BUFEE ambapo kwa 15K unapata 10GB..... Ndiyo nayoiona ni nafuu kwangu kwa sasa.
 
Si alisema tukijiunga bando , tunaenda kuangalia ma-video ya ajabu ajabu

Wenye kazi zinazotegemea internet tumeacha

1 GB Ni 3000 , wakati juzi tu ilikuwa Elfu 1 una-download zaidi ya 6 GB - Halotel
 
Hapo kabla Halotel walikuwa wanatoa unlimited kwa 1500 6-12 unaweza kushusha hata gb200 bila shida.
Ila kwa sasa hakuna mtandao unaotoa vifurushi vya usiku.
 
Natumia Voda, kuhusu kula bando kihalali hata Voda wanakula kihalali. Natumia App ya Internet Meter inanionyesha matumizi ya mb ambayo simu yangu inatumia. Hesabu za mb zinaenda sawa kabisa na za mtandao. Ishu saivi ni mitandao ya kijamii ambayo watu wanatumia sana inakula sana mb, Instagram, Tik Tok n.k
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…