Msaada: NIlianza kuumwa malaria, ikaja Typhoid, na sasa ni bacteria kwenye njia ya mkojo

Msaada: NIlianza kuumwa malaria, ikaja Typhoid, na sasa ni bacteria kwenye njia ya mkojo

tindikalikali

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2011
Posts
4,854
Reaction score
1,129
Kwanza nawasalimu wote!

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, tatizo langu lilianza mwaka 2009/2010! Nakumbuka niliumwa, nikaenda dispensary nikaambiwa nina Malaria, nilipewa dawa..nilitumia lakini sikuona nafuu! Baada ya mwezi nilienda kupima nikaambiwa nina malaria tena, nikapewa dawa na ikawa hivyo karibia kila mwezi!

Nilitumia dawa nyingi sana, pia nilijitahidi kutumia chandarua ila bado nikawa muhanga wa malaria ya mara kwa mara! Mwaka 2010 mwishoni nilikuwa na daktari akashauri nilazwe niwekewe drips za quinin..nililazwa kwa siku tatu..nikaruhusiwa ila hali haikubadilika, hata nilipoenda kupima tena niliambiwa nina malaria..hali hiyo ilienda mpaka 2011/2012 ambapo nilikuja humu kuomba suluhu la tatizo langu, nilikuta topics nyingi sana za Malaria...kuna mdau alishauri ninunue dawa ya kihindi inaitwa Zandu, kiukweli Zandu ilinisaidia na Malaria ikawa mwisho wake!!

Mwisho wa malaria ukawa mwanzo tatizo jingine, typhoid na minyoo vikaanza kunisumbua..nimetumia dawa nyingi..nikawa napona ila sirudi katika ile hali ya mwanzo! Kuna wadau humu walinishauri nikafanye vipimo hospital kubwa, 2013 nilienda Regency...walichukua vipimo kadri walivyoona inafaa, mwisho wa siku daktari akadai sina tatizo lolote, nilimwambia lakini mimi naumwa..akanambia haiwezekani uumwe zaidi ya miaka miwili na uendelee kuishi, ungekuwa ushakufa!

Maisha yaliendelea huku mwilo ukiwa dhoofu, kazi za watu ikawa ngumu kufanya hali iliyopelekea kuacha kazi na kuamua kujiajiri!! Bado huku kwenye shughuri zangu nashindwa kuzifanya kwa ufanisi, pesa nyingi nazitumia katika kujitibu..maana haijawahi pita mwezi nikawa nipo salama kabisa!!

Mwaka huu nimefanya checkup ya HIV, January, April na May na matokeo yakawa negative! Ila bado hali ya mwili ni ile ile!

Hivi majuzi nimepima, nikaambiwa nina bacteria kwenye njia ya mkojo..nimepewa dozi ya Azuma..nimemaliza dozi ila hakuna nafuu yoyote, hapa tupo linasumbua..na muda wote najisikia kulala tu!

Wadau nateseka na hii hali, sijawahi lazwa hospital toka 2010, wala sijawahi umwa kiasi kwamba nikahitaji usaidizi wa mtu mwingine! Najitahidi kufata kanuni zote za usafi, ila hali ndo hiyo!

Najua humu kuna madaktari, na watu waliopitia hali kama yangu..naombeni msaada wenu ili nami niweze angalau kufurahia haya maisha!!

Natanguliza shukrani!!
 
Pole sana mkuu, watakuja wataalam humu watakusaidia
 
Fika tabata Aroma
kuna mchina mmoja hivi hapo Aroma House
muone na akikupa dawa kunywa halafu ulete mrejesho
 
Ngoja wadau waje naamini watatoa mawazo mbadala. But the key is to deny that sickness by faith. Faith heals
 
Kwanza nawasalimu wote!..........

Hivi majuzi nimepima, nikaambiwa nina bacteria kwenye njia ya mkojo..nimepewa dozi ya Azuma..nimemaliza dozi ila hakuna nafuu yoyote, hapa tupo linasumbua..na muda wote najisikia kulala tu!

Wadau nateseka na hii hali, sijawahi lazwa hospital toka 2010, wala sijawahi umwa kiasi kwamba nikahitaji usaidizi wa mtu mwingine! Najitahidi kufata kanuni zote za usafi, ila hali ndo hiyo!

Najua humu kuna madaktari, na watu waliopitia hali kama yangu..naombeni msaada wenu ili nami niweze angalau kufurahia haya maisha!!

Natanguliza shukrani!!

Nakushauri kama ukienda hospitali,na wewe jitahidi kujitutumua kidogo na umpe ushauri daktari ili umuongezee wigo/uwezo wa kukupa vipimo na tiba sahihi.

Kwa harakaharaka tu nahisi yafuatayo:

1.Kuna uwezekano huli vizuri.
2.Kuna uwezekano hunywi maji ya kutosha.
3.Kuna uwezekano una tindikali/sumu nyingi kwenye damu.Hivyo unaweza kucheki pH ya damu/mwili wako kama iko sawasawa.Na hili ndilo hasa linaweza kuwa tatizo lako la msingi.Umetumia dozi nyingi tofauti zenye kemikali tofauti kwa muda mrefu,hivyo kuna uwezekano sumu imejirundika mwilini na ndio inayokusumbua.Kama una tindikali nyingi kwenye damu huwezi kujisikia vizuri na wakati mwingine unaweza kupimwa lakini wasione ugonjwa mwilini.

Hebu jaribu kucheki hilo namba 3 kwanza halafu uje tena hapa kutujuza.Vinginevyo penda kula vizuri(vyakula bora/vya asili zaidi) na kunywa maji ya kutosha(si chini ya lita 2 kwa siku).Ukifanya mazoezi ya kukutoa jasho pia ni vyema zaidi.

Fahamu kwamba tindikali/acid kwenye damu ni sumu.
 
pole sana,Mungu yupo pamoja naww,usisahau kumuomba kadr uwezavyo,na kama wewe ni muslim,fanya dhikr sana
 
Nakushauri kama ukienda hospitali,na wewe jitahidi kujitutumua kidogo na umpe ushauri daktari ili umuongezee wigo/uwezo wa kukupa vipimo na tiba sahihi.

Kwa harakaharaka tu nahisi yafuatayo:

1.Kuna uwezekano huli vizuri.
2.Kuna uwezekano hunywi maji ya kutosha.
3.Kuna uwezekano una tindikali/sumu nyingi kwenye damu.Hivyo unaweza kucheki pH ya damu/mwili wako kama iko sawasawa.Na hili ndilo hasa linaweza kuwa tatizo lako la msingi.Umetumia dozi nyingi tofauti zenye kemikali tofauti kwa muda mrefu,hivyo kuna uwezekano sumu imejirundika mwilini na ndio inayokusumbua.Kama una tindikali nyingi kwenye damu huwezi kujisikia vizuri na wakati mwingine unaweza kupimwa lakini wasione ugonjwa mwilini.

Hebu jaribu kucheki hilo namba 3 kwanza halafu uje tena hapa kutujuza.Vinginevyo penda kula vizuri(vyakula bora/vya asili zaidi) na kunywa maji ya kutosha(si chini ya lita 2 kwa siku).Ukifanya mazoezi ya kukutoa jasho pia ni vyema zaidi.

Fahamu kwamba tindikali/acid kwenye damu ni sumu.

Asante mkuu, maji najitahidi kunywa..japo kwenye kula sina ratiba maalumu maana naishi peke yangu! Maji nakunywa, ila mazoezi niliwahi anza ila nikajikuta nashindwa kulingana hali yangu!!

Nitapima hiyo PH then nitaleta mrejesho!!

Pia hizo sumu nini suluhisho lake, niliwahi kutana na watu wanadai wanatoa sumu kwa mashine(sina hakika kama ni kweli na inawezekana), walinifanyia process yao bado sikuona mabadiliko!!
 
pole sana ndugu,nadhai umepewa ushauri wa kutosha,ila nami naongezea kwamba yote yakishindikana,mualike Mungu mwenyewe ashughulike,maana pale uwezo wetu unapoishia yeye huanzia hapo,Yesu aweza kukuponya haijalishi dini yako
Kwanza nawasalimu wote!

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, tatizo langu lilianza mwaka 2009/2010! Nakumbuka niliumwa, nikaenda dispensary nikaambiwa nina Malaria, nilipewa dawa..nilitumia lakini sikuona nafuu! Baada ya mwezi nilienda kupima nikaambiwa nina malaria tena, nikapewa dawa na ikawa hivyo karibia kila mwezi!

Nilitumia dawa nyingi sana, pia nilijitahidi kutumia chandarua ila bado nikawa muhanga wa malaria ya mara kwa mara! Mwaka 2010 mwishoni nilikuwa na daktari akashauri nilazwe niwekewe drips za quinin..nililazwa kwa siku tatu..nikaruhusiwa ila hali haikubadilika, hata nilipoenda kupima tena niliambiwa nina malaria..hali hiyo ilienda mpaka 2011/2012 ambapo nilikuja humu kuomba suluhu la tatizo langu, nilikuta topics nyingi sana za Malaria...kuna mdau alishauri ninunue dawa ya kihindi inaitwa Zandu, kiukweli Zandu ilinisaidia na Malaria ikawa mwisho wake!!

Mwisho wa malaria ukawa mwanzo tatizo jingine, typhoid na minyoo vikaanza kunisumbua..nimetumia dawa nyingi..nikawa napona ila sirudi katika ile hali ya mwanzo! Kuna wadau humu walinishauri nikafanye vipimo hospital kubwa, 2013 nilienda Regency...walichukua vipimo kadri walivyoona inafaa, mwisho wa siku daktari akadai sina tatizo lolote, nilimwambia lakini mimi naumwa..akanambia haiwezekani uumwe zaidi ya miaka miwili na uendelee kuishi, ungekuwa ushakufa!

Maisha yaliendelea huku mwilo ukiwa dhoofu, kazi za watu ikawa ngumu kufanya hali iliyopelekea kuacha kazi na kuamua kujiajiri!! Bado huku kwenye shughuri zangu nashindwa kuzifanya kwa ufanisi, pesa nyingi nazitumia katika kujitibu..maana haijawahi pita mwezi nikawa nipo salama kabisa!!

Mwaka huu nimefanya checkup ya HIV, January, April na May na matokeo yakawa negative! Ila bado hali ya mwili ni ile ile!

Hivi majuzi nimepima, nikaambiwa nina bacteria kwenye njia ya mkojo..nimepewa dozi ya Azuma..nimemaliza dozi ila hakuna nafuu yoyote, hapa tupo linasumbua..na muda wote najisikia kulala tu!

Wadau nateseka na hii hali, sijawahi lazwa hospital toka 2010, wala sijawahi umwa kiasi kwamba nikahitaji usaidizi wa mtu mwingine! Najitahidi kufata kanuni zote za usafi, ila hali ndo hiyo!

Najua humu kuna madaktari, na watu waliopitia hali kama yangu..naombeni msaada wenu ili nami niweze angalau kufurahia haya maisha!!

Natanguliza shukrani!!
 
Mkuu kama iman yako inaruhusu......jarbu na miti shamba..
Magonjwa mengne c ya hospital
 
Asante mkuu, maji najitahidi kunywa..japo kwenye kula sina ratiba maalumu maana naishi peke yangu! Maji nakunywa, ila mazoezi niliwahi anza ila nikajikuta nashindwa kulingana hali yangu!!

Nitapima hiyo PH then nitaleta mrejesho!!

Pia hizo sumu nini suluhisho lake, niliwahi kutana na watu wanadai wanatoa sumu kwa mashine(sina hakika kama ni kweli na inawezekana), walinifanyia process yao bado sikuona mabadiliko!!

hebu kunywa juicy ya limao kwa wiki mbili uone....
tatizo lako linaweza kuwa linaitaji tiba mbadala kuliko kujilundikia dose za typhod kila mwezi mwilini,,,,,
limao linasaidia kuondoa sumu mwilini...,jaribu matunda ,mbogamboga,salad etc viwe sehemu kubwa ya diet
 
Pole sana mkubwa. Samahani kama takuingilia imani yako; nenda kwa waganga wa jadi ila usiende kupiga ramli. Fika hapo mpe hiyo historia binadamu hawana wema. Dada yangu aliwahi kuamka amenyolewa nywele zote na chale mwili mzima akafuatiwa na maumivu ya kichwa kila mara ilifikia hatua tukapata msaada wa upande wa dawa za kienyeji na hadi sasa sister mzima tele na mume wake.
 
Pole sana Mkuu tindikalikali,Mungu atakusaidia pia jaribu kuzingatia shauri utakazopewa humu.ni huzuni sana mtu unapokuwa mgonjwa ukatumia dawa usipone unapata msongo mkali sana wa mawazo nayo yaweza kuchangia hali yako..jitahidi(japo ni vigumu) kuikataa hiyo hali ktk nafsi yako jione wewe ni mzima kama watu wengine pia omba Mungu akuponye coz mkono wake na uwezo wake hufika pale binaadam anapoona hana plan B.ugua pole Bro.
 
Last edited by a moderator:
hebu kunywa juicy ya limao kwa wiki mbili uone....
tatizo lako linaweza kuwa linaitaji tiba mbadala kuliko kujilundikia dose za typhod kila mwezi mwilini,,,,,
limao linasaidia kuondoa sumu mwilini...,jaribu matunda ,mbogamboga,salad etc viwe sehemu kubwa ya diet

Mkuu hiyo juice ya limao nakunywa kwa kipimo gani!? Je ni mara ngapi kwa siku!?
 
Mkuu kama iman yako inaruhusu......jarbu na miti shamba..
Magonjwa mengne c ya hospital

Mkuu mimi sina tatizo na mitishamba, nshajaribu..ila wengi nao wapo kibiashara zaidi!! Labda kama nitapata mahala sahihi kwa ajiri ya hiyo tiba!!
 
Back
Top Bottom