Kwanza pole na Michosho ya NACTE kukupangia mahali ambapo hukupenda. Pole sana.
Pili,hii ishu yako ingetakiwa iwe jukwaa la Elimu na wala siyo Jukwaa la JF Doctors. Hili jukwaa ni specific kwa kutoa elimu mahususi kuhusu Afya ya jamii,tiba na magonjwa yanayowanyemelea watu na hatua za kuchukua.
Wewe hilo lako halihusiani na afya au maradhi.
Tatu,hiyo ni kozi kam kozi nyingine tu. Hapo unaenda kusoma Udaktari wa Wanyama. Uzuri umepangiwa chuo standard kwenye kozi husika. Ni kozi nzuri na kama utaendelea vema baadae ukajiendeleza utasoma Shahada ya mambo ya mifugo pale Sokoine University (SUA). Ajira zake zipo na zinalipa.
Lakini zaidi fata kitu kipendacho roho. Kama hupendi mifugo basi achana na hiyo kozi. Tafuta jinsi uende ukasome chuo kinachotoa Kozi za afya kama Clinical Officer au Uuguzi.
Mwisho nikutakie kila la kheri.