Msaada: Nimekula maboga nimevimbiwa nifanyeje?

ndupa

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2008
Posts
4,403
Reaction score
148
Habari za asubuhi,

Ni kwamba niko ugenini pande za wasukuma huku vijijini Kilimatinde ndani kabisa,sasa katika kuamka asubuhi imeandaliwa breakfast ya maboga na maziwa ya mgando.

Sasa katika kuwaiga wenyeji nikaparamia maboga matatu na maziwa lita moja .Wakati Mjini kwa bigdady nimezoea kiepe sahani moja niko vizuri nilivopiga boga moja nikawaambia asante wakasema acha kutania tumbo sasa ikabidi niendeleze matatu.

Hapa ninapoongea nimetoka chooni nimekaa zaidi ya nusu saa nakamua mzigo hautoki naishia kupumua tu.
Nimerudi katika chumba yangu nimelala tu ukitegemea mwenye duka la madawa kaenda kanisani mjini.

Nifanyeje maana tumbo lauma full kuunguruma tu bu bu bu bu.
 
Mkiitwa wanaume wa dar mnalalamika!!! Sasa mwanaume mzima unakulajr kiepe?? Ona yaliyokukuta sasa!!! Nakushauri ubaki huko huko ili usahau maisha ya kiepe na fanta!!!
 
mkiitwa wanaume wa dar mnalalamika!!! Sasa mwanaume mzima unakulajr kiepe?? Ona yaliyokukuta sasa!!! Nakushauri ubaki huko huko ili usahau maisha ya kiepe na fanta!!!
acha kabisa
 
Maboga matatu ama vipande vitatu vya Maboga? Kama ni Maboga matatu basi wewe ni kiboko.
 
Meza dulcolax , zauzwa maduka ya dawa ...
 
Mmmmh,hayo majanga.
Kwan hukujua hata huyo msukuma akija Dar ukampa hicho kiepe nae atavimbiwa japo sio kwa kiwango chako cha maboga?!.
NGOJA TUSUBIRI WANAKUJA KUKUSHAURI WAJUMBE WENGINE mimi umenishinda uwezo!.
 
Meza dulcolax , zauzwa maduka ya dawa ...

Ushaambiwa muuza duka la dawa kenda kanisan,mpen another alternative.
But hajawa wazi,kwa hali ya kawaida kwa binadam kula maboga matatu na lita ya maziwa mgando ni jambo la kustaajabisha NA kuvimbiwa ni habari nyingine ambayo ni lazima ikukute
 
Ushaambiwa muuza duka la dawa kenda kanisan,mpen another alternative.
But hajawa wazi,kwa hali ya kawaida kwa binadam kula maboga matatu na lita ya maziwa mgando ni jambo la kustaajabisha NA kuvimbiwa ni habari nyingine ambayo ni lazima ikukute

Kama hadi mda huu kavimbiwa na hajanya basi aende hospitali, na mda atakuwa anajambia mdomoni kwa kihaya tunasema 'kutela empii' '
 
Jitahidi kujamba mara nyingi uwezavyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…