Msaada: Nina Cyst kwenye ovary ya kulia

dash m

Member
Joined
Mar 29, 2015
Posts
81
Reaction score
7
Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 28, nimeolewa na nina mwaka sasa ila sijashika mimba. Ninahitaji kupata mtoto.

Nimekwenda kupima nikaambiwa nina fangasi kwenye njia ya uzazi na cyst kwenye ovary ya kulia. Anayejua dawa ya kutoa cyst bila ipasuaji, naomba msaada. Na je, naweza kupata mimba nikiwa na hizo cyst?
 
Unaweza kuconceive, cyst huwa ni hormanal, inatokea na wakati mwingine haitokei. Kuhusu fangasi, pata matatibu sababu fangasi au infection kwenye kizazi ni chanzo kikuu cha kuzuia mimba kutunga.

USHAURI: nenda kwa Dr Mwaka, amesaidia wengi sana nina ushuhuda kwa hilo na watu wengi tu. Muombe Mungu kwa imani naye atatenda, hakuna asiloweza, yote kwake yanawezekana kwa imani.
 
Ningekusaidia, ila kwakuwa wengi wetu siku hizi tunaamini njia za tiba ya asili ni utapeli na ushetani inabidi uende huko huko hospitali mpaka utakapo pata tiba sahihi.
Pole sana Mkuu, Mungu wa mbinguni ainusuru ndoa yako ampe uvumilivu mwenzi wako.
 
Ningekusaidia, ila kwakuwa wengi wetu siku hizi tunaamini njia za tiba ya asili ni utapeli na ushetani inabidi uende huko huko hospitali mpaka utakapo pata tiba sahihi.
Pole sana Mkuu, Mungu wa mbinguni ainusuru ndoa yako ampe uvumilivu mwenzi wako.

Ni kweli kabisa umenena vyema kabisa wengi wanaona hayo mambo ni ya kishetani wakati wengi tu wanasaidiwa kwa mambo mengi tu na wanafanikiwa kiongozi.

Wengi wanasema BANIANI mbaya lakini kiatu chake dawa.Pole sana kwa dada yetu.
 
Mimi sichagui tiba wapendwa...kama unaweza kunisaidia
 
Tibu hizo fungus kwanza coz ni hatari. Hizo cyst zisikutishe coz mimi nina marafiki wengi wana watoto now na wao walikua na cyst, but walipata mimba. Cyst kila msichana anayefikia age ya kuzaa anapata, sema huwa zinayeyuka zenyewe na baadhi huwa haziyeyuki sasa hapo ndipo inapopelekea upate huo uvimbe sababu cyst yako haijayeyuka.

Wengine wanazo lakin hawana dalili za nje na wengine wanapata dalili kama kuumia wakat wa hedhi. Na wakati wa kufanya tendo unahis maumivu hata raha hupat unaona unachoshwa tu. Wengine inafikia kipindi kichefu chefu. Kula wanakula kidogo sana anakosa appetite ya kula.

Hayo ni machache tu lakin cha msingi tibu fungus nahis hao wanaua mbegu zinazo ingia ukisha tibu hapo kapime if zimeisha. Hapo anza kusaka mtoto sasa. Utapata mtoto tu na once unapo jifungua cyst hutoiona again . mm siyo Dr nimejaribu tu kukushaur ngoja wataalamu waje kikubwa hebu muombe Mungu zaid.
 
Unaweza pata mtoto na usiwe na wasiwasi. Mimi sio daktari ila ninafahamu kwakuwa mke wangu alikuwa na tatizo hilo na baada ya matibabu sasa ameweza kupata watoto. Bila kulitibu huwezi pata watoto kwakuwa cyst in damage embryo. Inatakiwa utaalamu wa hali juu kuiondoa na kubakisha nyama inayoweza kupokea na kutunza mimba.

Yeye alifanyiwa LAPARASCOPE nchini Uturuki, sina uhakika kama tunafanya procedure hiyo Tanzania kwa sasa na kwa utaalam kiasi gani. Yeye alivyofanyiwa ndani ya miezi miwili tukafanya ivf na akapata mimba ya Twins.

Ukitaka zaidi msaada toka kwangu nitaangalia jinsi gani ya kuwasaidia na mumeo ila Muumba aweze kuwajaaliwa watoto.
 
Mimi sichagui tiba wapendwa...kama unaweza kunisaidia

Ok Mkuu, rudi kwanza hospital utibu hizo fangasi, kisha rudi tena kwenye zoezi la kutafta mtoto. Usipompata ndani ya siku60 uje na mwenza wako PM tutajadili pamoja nini kifanyike.
Hakuna gharama ktk kipindi chote utakapokuwa unatumia dawa. Ila utatoa asante baada ya kumpata huyo baby wenu.
 

Ni dawa gnu nzur za fangaasi mana naona nimetumia nyingi bila mafanikio
 

Sante sana..kdogo napata matumain
 

Sante dana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…