Msaada: nina Typhoid nimemeza dawa hazijasaidia, nina tatizo la kutokunywa maji

cleokippo

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2014
Posts
2,118
Reaction score
1,797
Wana Jf,

Mimi nilienda kupima, nikakutwa nina Typhoid, nikaandikiwa dawa nikaenda kununua cpro vidonge 20 nikatumia kwa muda wa siku 10, baada ya kumaliza doz, sikupata matokeo mazuri.

Yaan hali ilikuwa iko vilevile, ikabidi nirudi kwenye maabara ile ile nikawaeleze kuhusu hilo tatizo ili kama ikiwezekana niangalie tena kama ipo au imekwisha, wakaniambia vipimo vitadanganya inabidi nikae miezi 3 ndio nipime tena typhoid, ila wakanishauri ni check mkojo na Malaria.

Nikafanya hivyo kama walivyonishauri ikaonekana nina wadudu watatu, nikameza Malafin, ila pamoja na kumeza Malafin bado tena hali iko vile vile.

Sasa hapo tatizo nini? Vipimo vingine nilivyofanya ni HIV, BP, SUKARI vyote hivyo viko safi, na tatizo langu kubwa sinywi maji kabisa, naweza nikakaa hata siku mbili sijanywa maji. Nombeni msaada wenu.

Ahsanteni sana.

Nawasilisha.
 
Madaktar!

Mimi ninatatizo la kutokunywa maji kabisa, yaani nina uwezo wa kukaa hata siku mbili bila kunywa hata kikombe kimoja cha maji.

Sasa nauliza tiba ya hii kitu ni ipi?
 
Nashkuru kwa ushaur wako tallent, sasa hapa cjajua ni dawa gan zilizoshindwa kufanya kazi, maana cjui kama bado ni typhoid malaria kwa kuwa dalili zinafanana
 
Maji ni tiba nzuri sana kunywa maji atleast 2lts kwa siku. Utaona tofauti
 
Dawa wanazokupa ni labda zime isha mataumizi au feki.
 
Tatizo lako la kiafya halitatatuliwa kamwe kama wewe hutatoa maelezo fasaha ya kile hasa kinachokusumbua kwa Daktari au Mganga.Jukumu la Daktari/Mganga ni kukusanya taarifa za ugonjwa wako kwa kuandika historia ya dalili za ugonjwa(signs and symptoms) kuzifanyia uchambuzi wa kitaalamu kukuchunguza wewe na kukupima,kuagiza vipimo vya damu,mkojo,choo kikubwa kulingana na dalili ulizonazo na kufikia uamuzi wa awali wa ugonjwa wako( provisional diagnosis) ambao utahitaji utafiti zaidi ili kujiridhisha kama kweli ndio chanzo cha tatizo lako la kiafya.Maelezo yako hayaonyeshi kilichokupeleka hospitali ni nini hasa(Main complain??),Unasema tu ulienda kupima ukaambiwa una tyhoid.

Hapa napata picha kuwa hukumuona Daktari/Mganga ila ulimuona mtu wa maabara akakupima,kama aliiona matokeo ya kipimo chako kuwa na tyhoid hiyo ni siri yake.

Yawezekana alitengeneza mkwanja kwa kuona wewe unafuata short cut zaidi kuliko kufuata utaratibu wa tiba wa kumuona Daktari/Mganga kwanza. Inaonekana pia tatizo lako ni kutokunywa maji,kama hicho ndio kilikupeleka hospitali ungefanya consultation kwa Daktari/Mganga zaidi kuliko kwenda kupima vipimo ambavyo havina uhusiano na ugonjwa wako.

Kutokunywa maji kunategemea na sehemu uliyoko;Baridi/joto hapa nalenga unatoka jasho sana au la,inategemea vyakula unavyokula vya maji maji kiasi gani,Labda unatumia juice zaidi,Uji,mtori?.

Yawezekana huweki sukari au chumvi nyingi pia.All in all mwili wako ndio unarekebisha mahitaji yako ya maji mwilini kulingana na mahitaji,wewe huwezi kujilazimisha kunywa maji kama hujisikii kufanya hivyo.'kuwa na kiu'. Kama tatizo lako bado halijapata ufumbuzi,Ushauri wangu "Kamuone Daktari/Mganga".
 
Nashkuru gwab kwa ushaur wako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…