nyakahanga
JF-Expert Member
- Mar 7, 2013
- 240
- 65
Salaam wakuu,
Mimi ni kijana mwenye kiu ya mafanikio lakini sina mtaji wa kutosha. Najitokeza kwenu kuomba msaada juu ya hii ishu.
Nimejaribu kufanya utafiti hapa Musoma na nimeona kuna vijana wengi wenye vipaji lakini wanaishia kuimbia "maghetoni" tu.
Hivyo nimeamua kuja na wazo la kuanzisha "Musoma Young Musicians Search" (MYMS) itakayojihusisha na kusaka vipaji vya kuimba na kurap kwa vijana wasiozidi miaka 20 watakaopitia mchujo hadi kubaki watano bora na ambao watazawadiwa zawadi mbalimbali ikiwemo kupelekwa studio na kusimamiwa kazi zao za muziki kwa kipindi kitakachokuwa stated kwenye mkataba.
Kama nilivyotangulia kusema hapo juu ni kuwa sina mtaji wa kutosha, ila nahitaji udhamini wa makampuni makubwa yanayopatikana hapa Musoma kama Cocacola (NBCL), Musoma Food, n.k. Hivyo naombeni ushauri wenu nianzie wapi Kuyaapproach makampuni haya na mengine yaweze kutoa udhamini.
Nahitaji sana msaada wenu wadau.
Nawasilisha
Mimi ni kijana mwenye kiu ya mafanikio lakini sina mtaji wa kutosha. Najitokeza kwenu kuomba msaada juu ya hii ishu.
Nimejaribu kufanya utafiti hapa Musoma na nimeona kuna vijana wengi wenye vipaji lakini wanaishia kuimbia "maghetoni" tu.
Hivyo nimeamua kuja na wazo la kuanzisha "Musoma Young Musicians Search" (MYMS) itakayojihusisha na kusaka vipaji vya kuimba na kurap kwa vijana wasiozidi miaka 20 watakaopitia mchujo hadi kubaki watano bora na ambao watazawadiwa zawadi mbalimbali ikiwemo kupelekwa studio na kusimamiwa kazi zao za muziki kwa kipindi kitakachokuwa stated kwenye mkataba.
Kama nilivyotangulia kusema hapo juu ni kuwa sina mtaji wa kutosha, ila nahitaji udhamini wa makampuni makubwa yanayopatikana hapa Musoma kama Cocacola (NBCL), Musoma Food, n.k. Hivyo naombeni ushauri wenu nianzie wapi Kuyaapproach makampuni haya na mengine yaweze kutoa udhamini.
Nahitaji sana msaada wenu wadau.
Nawasilisha