MSAADA: Nitawezaje kulipwa mishahara yangu iliyozuiliwa?

MSAADA: Nitawezaje kulipwa mishahara yangu iliyozuiliwa?

CAMANGA

Member
Joined
May 14, 2023
Posts
72
Reaction score
299
Najua humu ndani naweza kupata msaada wa namna ya kudai mishahara yangu iliyozuiliwa kwa muda wa miezi nane huku nikiendelea na kazi.

Mshahara wangu ulizuiliwa baada ya kutokuwepo kazini kutokana na kuugua wakati wa likizo. Baada ya kupona, nilirejea kazini na kuwasilisha ushahidi wa kidaktari kuthibitisha kuwa nilikuwa naumwa. Waliporidhika na ushahidi huo, wakanirudisha kazini. Hata hivyo, ilichukua miezi nane bila mshahara wangu kurejea. Baada ya miezi hiyo, mshahara ulianza tena kama kawaida. Nilielekezwa kuandika barua ya kudai mishahara ya miezi hiyo nane. Baada ya kuandika barua na kujaza fomu maalumu ya kudai malimbikizo (arrears), kila ninapokwenda kwa HR kuulizia, wanadai kazi yao ilishakamilika na malipo yapo mikononi mwa Hazina.

Nashindwa kuelewa hatua nyingine za kuchukua kwani mtu pekee ninaweza kumuulizia ni DHRO.

Nifanye nini? Na ni mbinu gani naweza kutumia, kwani pia kuna mishahara ya miezi ya mwanzo wa ajira yangu ambayo sijawahi kulipwa hadi leo.

Naomba msaada wenu. 🙏
 
Andika vizuri. Uliumwa wakati wa likizo alafu badae ukarudi kazini na Docs za kuthibitisha ugonjwa Ina maana likizo iliisha na bado ukawa mgonjwa hivo ukachelewa ku report kazini ?
 
Umeandika umepindisha pindisha sana. Tuelezee kama unamuelezea muajiri kama unataka ushauri.
 
Ndio mkuu nilichelewa kureport so nikawa na tuhuma ya utoro kazini
Ulipaswa kutoa taarifa ya kuwa unaumwa kuanzia siku ulipotakiwa urudi kazini kutoka likizo.

Hapo wangekuwa na taarifa zako na wangekupa ruhusa ya kuugua.

Sasa wewe ukakaa kimya wakakuhesabu kama mtoro.

Laiti ungetoa taarifa na kupewa ruhusa, mishahara yako isingezuiwa.
 
Miez nane nje ya Kazi by any means kwa Sheria za Tanzania ni kwamba wewe ulishajifukuzisha kazi.

And upo eligible kwa likizo ya ugonjwa siku 123 tu, baada ya hapo ni bahati tu wamekurudisha kazini.

Dai taratibu wasije wakakutimua mazima
 
Mkuu kama kweli hao utumishi walisha wasilisha nyaraka zako kunakohusika, subiri utalipwa tu. Malipo ya serikali Huwa hayapo fasta fasta kama kama unavyo tarajia. Hayo malipo yanaweza kuchukua hata miaka 3 kupata hiyo pesa Yako.
 
Najua humu ndani naweza kupata msaada wa namna ya kudai mishahara yangu iliyozuiliwa kwa muda wa miezi nane huku nikiendelea na kazi.

Mshahara wangu ulizuiliwa baada ya kutokuwepo kazini kutokana na kuugua wakati wa likizo. Baada ya kupona, nilirejea kazini na kuwasilisha ushahidi wa kidaktari kuthibitisha kuwa nilikuwa naumwa. Waliporidhika na ushahidi huo, wakanirudisha kazini. Hata hivyo, ilichukua miezi nane bila mshahara wangu kurejea. Baada ya miezi hiyo, mshahara ulianza tena kama kawaida. Nilielekezwa kuandika barua ya kudai mishahara ya miezi hiyo nane. Baada ya kuandika barua na kujaza fomu maalumu ya kudai malimbikizo (arrears), kila ninapokwenda kwa HR kuulizia, wanadai kazi yao ilishakamilika na malipo yapo mikononi mwa Hazina.

Nashindwa kuelewa hatua nyingine za kuchukua kwani mtu pekee ninaweza kumuulizia ni DHRO.

Nifanye nini? Na ni mbinu gani naweza kutumia, kwani pia kuna mishahara ya miezi ya mwanzo wa ajira yangu ambayo sijawahi kulipwa hadi leo.

Naomba msaada wenu. 🙏
Pole Sanaa

Nukuu ya baba wa taifa.
""UTII UKIZIDI SANAA HUZAA UOGA, UOGA UKIZIDI SANA HUZAA UNAFIKI NA KUJIPENDEKEZA NA MWISHO WAKE NI MAUTI""
 
Kwanza ww una bahati utakuwa umekutana na Afisa Utumishi Muungwana,kosa ulilolifanya ni la kufukuzwa kazi moja kwa moja.
By the way Mwambie HR wako mawasiliano ya approver wenu aliyoko Utumishi,huyo ndio anayepitisha kila kitu chenu cha kiutumishi atakuwa anajua shida ni nini.
Siku nyingine usirudie ujinga uliofunya utapoteza kazi ukiwa unaangalia.
 
Mleta mada ameandika maelezo yaliyonyooka kabisa tena yenye kueleweka, lakini wengi wa wachangiaji hapa JF mpaka sasa wameshindwa kabisa kuelewa na kuchangia mada husika kijinga kabisa. Kama JF ndio kioo cha watu wenye upeo mpana zaidi hapa Tz katika kuchambua mambo vyema mitandaoni, na hali ndio hii, basi taifa limekwisha kabisa.

Turudi kwenye mada....
Kwa kifupi kabisa, kwa hiyo hatua uliyofikia basi kwa 99% tegemea kulipwa haki zako, japokuwa zitachelewa, hakuna uhakika ni lini utalipwa na madai yako kwa sasa yako hazina. Kwa sasa mwajiri wako hana namna yoyote ya kuweza kukusaidia moja kwa moja kwa kuwa mkondo wa malipo upo upande wa hazina. Kitu pekee mwajiri angepaswa kufanya ni hiki:
1. Akupe barua ya kukueleza hatua ya madai yako ilipofikia (yaani madai yako kwa sasa yapo mikononi mwa hazina) na ikiwezekana kueleza mchanganuo wa madai yako aliyoyaidhinisha kwenda hazina. (Hii inatoa nafasi ya wewe kuwailiza hazina, kukumbushia au kuja kudai ikiwa utalipwa kwa upungufu nk)

2. Afisa utumishi kukupa uzoefu wa namna malipo ya hazina yanavyoweza kuchelewa au kuwahi.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Najua humu ndani naweza kupata msaada wa namna ya kudai mishahara yangu iliyozuiliwa kwa muda wa miezi nane huku nikiendelea na kazi.

Mshahara wangu ulizuiliwa baada ya kutokuwepo kazini kutokana na kuugua wakati wa likizo. Baada ya kupona, nilirejea kazini na kuwasilisha ushahidi wa kidaktari kuthibitisha kuwa nilikuwa naumwa. Waliporidhika na ushahidi huo, wakanirudisha kazini. Hata hivyo, ilichukua miezi nane bila mshahara wangu kurejea. Baada ya miezi hiyo, mshahara ulianza tena kama kawaida. Nilielekezwa kuandika barua ya kudai mishahara ya miezi hiyo nane. Baada ya kuandika barua na kujaza fomu maalumu ya kudai malimbikizo (arrears), kila ninapokwenda kwa HR kuulizia, wanadai kazi yao ilishakamilika na malipo yapo mikononi mwa Hazina.

Nashindwa kuelewa hatua nyingine za kuchukua kwani mtu pekee ninaweza kumuulizia ni DHRO.

Nifanye nini? Na ni mbinu gani naweza kutumia, kwani pia kuna mishahara ya miezi ya mwanzo wa ajira yangu ambayo sijawahi kulipwa hadi leo.

Naomba msaada wenu. 🙏
Leave ya ugonjwa nadhani ina documents zake , je unazo ?
 
Miez nane nje ya Kazi by any means kwa Sheria za Tanzania ni kwamba wewe ulishajifukuzisha kazi.

And upo eligible kwa likizo ya ugonjwa siku 123 tu, baada ya hapo ni bahati tu wamekurudisha kazini.

Dai taratibu wasije wakakutimua mazima
Yaani acha tu

Ingekuwa ni mfanyakazi wake wa shamba au house girl hayuko kazini miezi 8 ungesikia majibu yake
 
Najua humu ndani naweza kupata msaada wa namna ya kudai mishahara yangu iliyozuiliwa kwa muda wa miezi nane huku nikiendelea na kazi.

Mshahara wangu ulizuiliwa baada ya kutokuwepo kazini kutokana na kuugua wakati wa likizo. Baada ya kupona, nilirejea kazini na kuwasilisha ushahidi wa kidaktari kuthibitisha kuwa nilikuwa naumwa. Waliporidhika na ushahidi huo, wakanirudisha kazini. Hata hivyo, ilichukua miezi nane bila mshahara wangu kurejea. Baada ya miezi hiyo, mshahara ulianza tena kama kawaida. Nilielekezwa kuandika barua ya kudai mishahara ya miezi hiyo nane. Baada ya kuandika barua na kujaza fomu maalumu ya kudai malimbikizo (arrears), kila ninapokwenda kwa HR kuulizia, wanadai kazi yao ilishakamilika na malipo yapo mikononi mwa Hazina.

Nashindwa kuelewa hatua nyingine za kuchukua kwani mtu pekee ninaweza kumuulizia ni DHRO.

Nifanye nini? Na ni mbinu gani naweza kutumia, kwani pia kuna mishahara ya miezi ya mwanzo wa ajira yangu ambayo sijawahi kulipwa hadi leo.

Naomba msaada wenu. 🙏
Polee saaa mkuu, mwambie hr akuonyeshe japo mchanganuo wa hayo malipo itakavokuwa , then upatapo mda jarbu kwenda hazna mwenyewe. Lakin mshukuru Mora kwa kurud mzigoni.
 
Embu tulia chapa kazi,,mambo ya hospitali unaweza foji pia,,Umepewa fea mnoo tulia.
 
Miez nane nje ya Kazi by any means kwa Sheria za Tanzania ni kwamba wewe ulishajifukuzisha kazi.

And upo eligible kwa likizo ya ugonjwa siku 123 tu, baada ya hapo ni bahati tu wamekurudisha kazini.

Dai taratibu wasije wakakutimua mazima
Hizo siku 123 umezitoa wapi mkuu!?,Mimi najua standing order inasema ni miezi 6 full payment,na baada ya hapo 6 months half payment na baada ya hapo tena unasitaafishwa
 

Attachments

  • Screenshot_20241014-202637.png
    Screenshot_20241014-202637.png
    108.1 KB · Views: 10
Back
Top Bottom