Msaada: Nyoka wananimalizia mayai ya kuku wangu

Msaada: Nyoka wananimalizia mayai ya kuku wangu

KIUNGOMCHEZESHAJI

Senior Member
Joined
Oct 4, 2013
Posts
120
Reaction score
255
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu.
Ninafuga kuku wa kienyeji hapa shambani kwangu. Kwa kweli kuku wanastawi vizuri na nilishaanza kufurahia matunda ya jasho langu, lakini ghafla nilianza kuona mayai yakipungua wakati kuku wanataga kila siku. Niliamini pasipo na shaka itakuwa nyoka. Hivi majuzi tukafanikiwa kumdaka nyoka mkubwa akiwa amemvamia kuku anayelalia. Kuku alianza kupiga kelele usiku ndipo tulipokurupuka na kwenda kuangalia, tukamkuta ameshameza mayai mawili tayari. Tulifanikiwa kumwua huyo nyoka.

Lakini hata baada ya kumwua huyo nyoka, bado mayai yameendelea kupungua. Pamoja na jitihada za kumwaga mafuta ya taa mlangoni na maeneo yanayozunguka nyumba lakini ufanisi ni mdogo. Hii mbinu ya kumvizia nayo ni ya kubahatisha. Je naweza kutumia mtego gani kuwamaliza nyoka shambani mwangu? Au nitumie dawa gani?
 
Hivi nawaza nikichukua yai nikatoboa kidogo nikaingiza sumu ya panya. Huyo nyoka atakula? Hebu jaribu hii. Toboa kwa ustadhi ingiza sumu ndani ya yake. Pia wanasema ukilichemsha yai halafu umamtegea. Kwa kuwa analimeza halitakaa lipasuke au kuyeyuka na atakufa.
 
Huyo ni nyoka MTU
Hapo naona sio nyoka bali kuna mtu anaiba hayo mayai
Nilikuwa na kuku wengi sana na kulikuwa na joka kubwa sana ambalo ni la miaka lakini hata siku moja hajala mayai
Na ni msaidizi mzuri sana kwa vibaka kwani wanajua uwepo wake hapo na hawasogei
Asubuhi huwa anaota jua kwenye barabara ya kuingilia shambani
We achana na nyoka mwizi yupo hapo mvizie tu


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Kapicha kidogo tuone hayo mazingira ili tujue ni njia gani ya kutumika pia itatusaidia kufahamu pia wadudu wengine wapenda mayai maeneo yako kama kenge...
 
Back
Top Bottom