Msaada Pumu ya ngozi (Eczema dermatitis)

Hata mimi pia sina amani na nakosa kujiamini kwa sababu siwezi vaa nguo kata mikono hata kuwe na joto sana.full vikoti tu.
 
mungu akutie wepesi, dawa za asil ushajaribu?
Nmeshajaribu altenative nyingi sana,nimepaka dawa nyingi sana bila mafanikio

Imebidi nianze kusoma soma mambo ya madawa ya ngozi huenda nitagundua kitu lakini wapi ?

Nmeshaenda kujaribu kufanya blood cupping au kupiga hijama,hili ni zoezi la kutoa damu chafu mwilini lakini wapi.
 
Naomba msaada unipe gharama za hizo dawa za kupaka na ambazo ni nzuri na mie nitumie.
 
Naomba msaada unipe gharama za hizo dawa za kupaka na ambazo ni nzuri na mie nitumie.
Hio Gentriderm(inauza sh 3000) ni nzuri inasaidia kuondoa ugonjwa unapopaka kwenye eneo husika,isipokua changamoto yake ni kama cream inakufanya unakua mweupe sasa mimi ni mtoto wa kiume naipaka usoni kwa nadra nikiona ugonjwa unazidi.

Pia nimewahi soma uzi humu unahusu mafuta ya nazi au mzeituni baada ya kuyachunguza risk zake nikaona yanaweza nifaa ndo nayatumia mpaka sasa kiujumla ni mafuta mazuri kwa ngozi yanaipa unyevu ngozi yangu ambayo ni kavu kavu hivi(wanasemaga matatizo haya ya kuwashwa yanatokana na ngozi kavu ko mafuta yanayoleta unyevu kidogo yanasaidia),mafut aya nazi yanauzwa sh 2500

Pia kuna dawa inaitwa betaderm ni tube zipo za aina mbili kuna ya ngozi kavu na ya ngozi nyevu ya ngozi kavu ni nyeupe ina rangi kama ya maji ndo naitumia mimi sasa hivi inatibu tatizo ila kidogo ugonjwa unakua na usugu na dawa

Na ya ngozi nyevu ni nyeupe rangi kama maziwa hii inawafaa watu wenye ngozi nyevu nyevu sikumbuki vizuri ila gaharama zake ni kama sh 4000.

Kuhusu sindano na hizo dawa za kumeza nakushauri ukawaone madakitari kwanza kaka
 
Mimi walivyonipima allergy walinichanja chale nyingi sana mkononi,kama 30 hivi ,halafu kuna matone ya kimiminika wakawa wananidondoshea waliponichanja,nikawa nahumuka na kuvimba then dokta akawa anaangalia ndo ananiambia mwili wangu unareact na vitu gani
 
Ndugu pole Kwa yanayokusibu

Nikusaidie Kwa kifupi

Mama yangu anagugua huu ugonjwa alifanikiwa kwenda kcmc

Kuna dawa n mafuta yako kama Aina tatu unapaka unapomaliza kuoga


Na pia zingatia haya

Usikae sehem zenye vumbi make sure vumbi halikugusi
Waeza nisaidia majina ya hayo mafuta tafadhali ?
 
Daah ahsante sana mkuu ubarikiwe.
 
Pole sana,dunia matatizo mengi.Ni mp nikupe ushauri.
Kama una nia ya kumsaidia mshauri hapahapa,yawezekana kuna wengine wanasumbuliwa na hayo matatizo,huoni Kama utakuwa umesaidia mkuu
 
Pole sana mm mwenyewe nilikuwa na hili tatizo nimesumbuka sana kama mwaka na zaidi hizo sindano za diprofos nimechomwa sana ila zenyewe unapona kwa muda alafu hali inarudi kama mwazo...kama upo da nakuomba uende tegeta kuna hospital inaitwa Rabinisia kama unatoka mwenge panda gar za bunju shuka kituo cha namanga ulizia watakuonyesha kuna dr wa ngoz pale huwa anafanya pale part time huwa anakuja siku za jumatatu na jumanne kuanzia saa kumi jion na anatibu watu 30 kwa siku hivyo kama unaenda jitahidi kuwahi maana ana watu wengi sana.....mm ndo nimeponea hapo pia huu ugojwa sio wa kupona kwa muda mfupi unahitaji muda sana....namba yangu kama unataka maelezo zaidi 0712106090 pole sana maana hata mm nimesumbuka sana na hiyo sio alegy ni pumu ya ngoz sasa dr wengi ambao sio watalaam wanakupa dawa za alergy na huku hiyo sio alergy...
 
Waeza nisaidia majina ya hayo mafuta tafadhali ?
Naomba kesho niyapige picha coz hayana jina yameandikwa tu matumizi Na jinsi yakuyatumia mama aliyapata kcmc alipokwenda kupata matibabu Na pia kuna majani yanaitwa mchakari unachemsha mizizi Na majani unakunywa Na kuoga maji yake yamemsaidia Kwa kiwango kikubwa sana naomba kesho inshallah nikutumie picha za hayo mafuta nivumilie
 
Prof mgonda amenisaidia sana Mimi pia Nina tatizo hilo hilo ninanafuu sasa
 
Nimekutumia pm hat a Mimi nikipata shida kama yako name kutibiwa hospital kwa dawa hizo hzo sikupona, nenda agha khan hospital dar mtafure prof mgonda atakusaidia sana Nimtkutumia pm mimj
 
nitashukuru sana
 
shkrani mkuu nitakutafuta
 

Pole sana ndugu achana an dawa za kizungu hazito kusaidia mimi ninakupa huduma ya kwanza tumia hii kila siku asubuhi unapo maliza kuoga jipake mafuta ya nazi sehemu yenye hayo maradhi asubuhi na usiku unapo lala tumia kila siku .Ukitaka Dawa ya kumaliza Maradhi yako nitafute kwa wakati wako.
Ukiwa na Shida yoyote ile
Usipo pona kwa Dawa za Hospitali nitafute mimi nipate kukutibia upate kupona ukihitaji matibabu yangu
Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe. fewgoodman@hotmail.com What's App na Viber +905344508169
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…