Msaada: Shamba lipo tayari kwa upandaji msimu wa March

J Mbungi

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2010
Posts
269
Reaction score
74
(NAOMBA MWENYE ROHO YA KUGUSWA ASICHOKE KUSOMA MAELEZO HAYA..MAAANA NI LAZIMA NIJIELEZE JAPO KIDOGO NDIO NIELEWEKE)

Samahani waungwana, Naamini badhayenu mtanielewa na atakayeguswa naomba anisaidie(Tusaidiane)

Nina shamba lka ekari 20(Bagamoyo njia ya Msata( Kijiji cha MASUGRU)..

Ni shamba jipya kabisa( Yaani nimefyeka msitu na kuanza kuandaa shamba kwa ajili ya kilimo cha Mahindi na Alizeti Msimu huu wa mwezi wa Tatu).

Kwa bahati Mbaya nimepata matatizo ya kifamilia kwenye huu mwezi ulio isha juziWa Pili)...Na kuyumba sana kipesa..Kwa kweli nilikuwa nipo katika hatua za mwisho za Kupanda(Maana na Mbegu tayari nimeisha iandaa).... Kwa bahati katikati ya mwezi wa pili mvua zime nyesha, na watu wengi waliweza kupanda, ila kwa kuwa mimi nilikuwa na matatizo sikuweza..

Sasa wiki jana ndio nimerudi na matatizo yamepoa kidogo..Sasa Nimeenda shamba kwa ajili ya utaratibu wa kupanda, lakini nimekuta majani/Mbegu za miti fulani hivi zimeota kwa kasi karibia sehemu kubwa ya Shamba..
Kwa maana hiyo aliwezi kupandwa mpaka sehemu hizo zipunguzwe majani...(Ili isiwe taabu kwenye palizi)

Kwa kusema ukweli ninahitaji nguvu kazi ya haraka( Kabla ya tarehe kumi na tano( Liwe tayari tena kwa ajili ya kupanda) .. Maana mvua za msimu zime anza na kufikia muda huo zitakuwazimechanganya kweli kweli...

MSAADA: NAOMBA MWENYE UTASHI WA KWELI NA ALIYEGUSWA NA HARAKATI ZANGU AWASLIANE NA MIMI MAPEMA IWEZEKANOVYO.. ILI TUWESZE KUZUNGUMZA NA KUKUBALIANA..

KIMSINGI.. NINA HITAJI UFADHILI WA SHILLING 1,00,000(MILIONI MOJA TU! KWA MAKUBALIANO MAALUMU( YAANI MKOPO WENYE RIBA YEYOTE ILE ILIMRADI NIPATE NAFASI YA KUTOSHA KABLA YA KUREJESHA MKOPO HUO) HATA KAMA RIBA NI ASILIMIA MIA MOJA)....

AU TUINGIE MAKUBALIANO KISHERIA KABISA( NIMKODISHE HILI SHAMBA YEYE ALIENDELEZE KUTOKEA LILIPOFIKIA..

NAMBA ZANGU: 0784 355775 (AU ANI- INBOX)..

AHSANTENI
 
Pole sana, hiki kipindi kuanzia decemba huwa kigumu sana, kuna fees, kodi, kulima hivyo kupata mtu utachelewa. Nakushauri kama ni mfanyakazi tafuta kampuni ukopee mshahara. Kama sio tumia collateral kama fenicha au card ya gari ukamalizie kulima. Pia kuna mbegu ya mahindi miezi mitatu nasikia decalb ni nzuri. Kwakweli wakulima kutokubaliwa mikopo kwa kuthamini ardhi zao ni kuturudisha nyuma sana. Mungu akusaidie.
 
Ubarikiwe sana MamaJoe kwa kunijibu na kujaribu kunipa ushauri..( I appreciate your Concern)..Nimejaribu mambo mengi mpendwa..Mpaka nilipofikia naona kama muda si rafiki kwangu..Ndio maana nikafikia hatua hii..Niporadhi kuingia makubaliano ya aina yoyote kwa mtu atakayeonyesha nia ya kunisaidia.. Namba zangu za simu +255784355775... Unaweza kuniunganisha na mtu yeyote tutajadiliana na kuona nini naweza fanya(Ikiwepo hata kulikodisha kwa mtu yeye akaliendeleza pale nilipofikia...Internet naingia mara chache kwasasa(Muda mwingi nipo kiguu na njia kutafuta ufumbuzi.. Kama kuna lolote jipya nitafute kwenye simu.. Ubarikiwe sana
 
Mkuu mbungi,Pole kwa yote hakuna kitu inaumiza km kuseti GOLI kisha ucfanikiwe inauma sn,mm yalinikuta Mwaka jana nililima EKA 18 nikapata AMBUSH ya Maisha nikashindwa kupanda nikakubali matokeo kwa Shingo upande bt mwaka huu namshukuru MUNGU niko sawax2! Kwa watz tulio wengi ningumu kusaidia maendeleo ya m2 ingekuwa sherehe sawa!, Ushauri wangu jaribu kuongea na NGUVU kz wakati unapambana kutafta PESA vijana waweSITE chakufanya nikuongea nao Vzr kdg utachokuwa unapata unawapa huenda ikakusaidia ili uckwame
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…