Msaada tafadhali maumivu ya mkono wa kushoto

Zuriel_cfc

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2017
Posts
4,092
Reaction score
9,063
Habari za leo wanajamvi..

Ninasumbuliwa sana na maumivu ya mkono wa kushoto yaani unauma hasa wakati wa usiku, sijajigonga mahali au kuulalia vibaya hapana umeanza tu kuuma muda sasa. Maumivu yanakuwa yanatembea hv na kama kufa ganzi fulani.

Je inawezekana nikawa na matatizo ya moyo?
Dawa za kuchua zinaweza kunisaidia?

Naomba msaada..
 
nenda hospitali chief,
ss hiyo dawa ya kuchua utaipaka mkono mzimaa!!?
 
Pole mkuu.
Mwone daktari kwa uhakika wa ushauri na matibabu.

Ila sio vibaya kwa yeyote jamvini hapa mwenye uelewa au taaluma ya udaktari akampa huduma ya kwanza (kimawazo) kaba ya kufika hosipitalini.
 
Pole mkuu.
Mwone daktari kwa uhakika wa ushauri na matibabu.

Ila sio vibaya kwa yeyote jamvini hapa mwenye uelewa au taaluma ya udaktari akampa huduma ya kwanza (kimawazo) kaba ya kufika hosipitalini.
Yap hicho ndo nilichokuwa nahitaji...
Asante kwa ushauri mkuu
 
Nenda hospitali mkuu
Jitahidi ukapima vipimo vya moyo hasa ECO.

Nenda pale tmj jumatatu na alhamisi jioni saa kumi na moja kuna clinic nzuri sana ya moyo kwa dr.shemu daktari bingwa wa moyo jakaya kikwete cardiac institute.
 
kuna vitu vya kufanya
01. mri ya shingo
02.echocardiogram to exclude cervical stenosis na heart problem
ukifanya hivi utakuja na nini ni tatizo
 
Una umri gani ndugu? Vpi kuhusu uzito wako?
 
30+ na nina 66kg
Ondoa wasiwasi hizo ni condition za kawaida sana, wala usianze kuwaza matatizo ya moyo. Hapo tafuta capsules piroxicam utumie siku tano hayo maumivu hauta yasikia, by the way usiache kufika hospital ili kujiridhisha
 
Ondoa wasiwasi hizo ni condition za kawaida sana, wala usianze kuwaza matatizo ya moyo. Hapo tafuta capsules piroxicam utumie siku tano hayo maumivu hauta yasikia, by the way usiache kufika hospital ili kujiridhisha
Sawa, nashukuru sana mkuu. Ubarikiwe
 
ondoa wasiwasi baada ya kufanya vipimo na na viseme negative......hiyo sio normal so usije ambiwa umechelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…