iron woman, hii kitu ni process ndefu. Ila njia ya kwanza ni kichunguza mzunguko wa hedhi(menstruation cycle),kubadilika badilika kwa mzunguko au ile damu inayotoka ikiwa na mabonge makubwa hapo yawezakana kuna tatizo.
UPIMAJI HOSPITALI UTAHUSISHA VITU VINGI MFANO;
njia za uzazi unazotumia,surgical history, lifestyle,medication history nk.
Pia unaweza ukachunguzwa tezi ya thairoid na matiti.
Kipimo kikubwa kitakachotumika ni ULTRA SOUND.
utachunguzwa Ovarian fuctioning,kuona ufanyaji kazi wa homoni za uzazi na kupima damu ili kujua kiasi cha INHIBIN B, hasa kipindi cha ovulation.
Pia uchunguzi hufanywa kupitia kwenye VAGINA(UKE).
Huko huangalia yale majimaji/utelezi uliopo kama unaweza kuruhusu mbegu za kiume zipite bila tatizo,kipimo huitwa POST COITAL TEST(PCT). pia utachunguzwa bacteria wanaokuwepo huko.
Ultrasound itatumika kuangalia upana wa ukuta wa uterus kama unaruhusu mimba kujishikiza, hii hasa hufanyika katika kipindi cha uvulation (siku za hatari wengi wanaita hivyo).
NJIA NYINGINE NI;
HYSTEROSALPINGOGRAM (HSG)- hii ni x-ray ya mfuko wa uzazi na mirija ya falopia inayopitisha mayai.
HYSTEROSCOPY- hapa kifaa kinaitwa Hysteroscopy kinaingizwa kupitia kwenye cervix(ukeni) mpaka kwenye mfuko wa uzazi(uterus) na docta anaangalia kama kuna tatizo lolote humo.
LAPAROSCOPY:- laparoscopy ni kifaa chembamba sana kama sindano, unachomwa kinaingia mpaka ndani,kina kamera hivyo dokta ataweza kuangalia mirija ya falopia(fallopian tubes) na uterus kama vipo sawa.
NB; Si lazima vipimo vyotr hivyo vitumike. Unaweza kuishia kwenye ultra sound, hivyo vingine hutumika ikiwa kuna wasiwasi juu ya majibu ya ultrasound au kupata uhakika zaidi..