Msaada tafadhalini Madocta wa JF

Edo Mashili

Member
Joined
Apr 19, 2015
Posts
24
Reaction score
0
Ndugu poleni na kazi kubwa ya kuimarisha afya za Watanzania pamoja na kujenga taifa.

Nina mdogo wangu wa kike ana umri wa miaka 20 ana tatizo linalompa shida sana,kuna vipele kama vchunusi vidogo vinamtokea miguun hasa maeneo ya kuanzia kwenye magoti kushuka chini vinavimba na kutoa usaha na vinaota kila baada ya dakika yani kiufupi vipo vingi sana na huwa vinamwasha sana.

Alipata dawa fulani kutoka kwa maduka ya wahindi ya kupaka na nyingine ya kuweka kwenye chai ila haijasaidia zaid vinaongezeka na vimeanza kumuuma sanaa. Ana wiki 2 toka aanze kuitumia iyo dawa ila hakuna mabadiliko.

Msaada tafadhalini wataalamu kwa mdogo vinamtesa sana.
 
Poleni Sana
Ngoja Wajuzi Waje Lakini Hospital Umekwenda?
 
nitafute kuna sabuni itamsaidia 0655731345
 
Hiyo nadhan ni haleji.. ! Ila jarb kumpekeka hospital ili ujue nn haswa kina msumbua
 
itakuwa ni allergy mkuu,either ya dawa au chakula fulani. . chunguza kama kuna dawa nyingine anazotumia, mara nyingi dawa zenye sulphur huwa na matatizo kama haya.
 
Mpatie vidonge vinaitwa cetrizine
Anakunywa kimoja kila siku
 
Edo Mashili

Edo bila kuona Picha ya hivyo vipele au Kuelezea kwa kirefu hali ya huyo mgonjwa inakuwa vigumu kukusaidia.
Kuna sababu zaidi ya 32 Zinazoweza kusababisha Hali hio kwa mgonjwa. Na kuna maswali mengi anatakiwa mgonjwa ayajibu na Test kidogo kabla ya kumshauri dawa ipi atumie.
Nakushauri uende kuonana na Daktari haraka iwezekanavyo.
 
Last edited by a moderator:
Mpatie vidonge vinaitwa cetrizine
Anakunywa kimoja kila siku

Wacha kabisa kushauri watu kutumia dawa Ovyo.
We unafahamu km mgonjwa ana kidney problems au porphyria ( rare inherited blood disorder) unaweza Kumdhuru na hio cetrizine?

Msipende kutoa ushauri bila kujali yatakayomkuta mgonjwa.
Ndio maana Kukawa na Hospitali na Madaktari sio kuambiwa tu na yyt kisha Ukaamua kutumia dawa bila vipimo.

Mtakuja kuua watu bure bure.
 

Mkuu sasa ndio unapiga za uso bila simile

Ni kweli nakiri kukosea, lakini nae huyu mbuloumundu kwa nini asiende kwa dakitari?
 
Mkuu sasa ndio unapiga za uso bila simile

Ni kweli nakiri kukosea, lakini nae huyu mbuloumundu kwa nini asiende kwa dakitari?

Mkuu Tatizo sio yeye.
Tatizo liko kwenye hali ya maisha.
Watu wengi hapo Tz wanatafuta tiba nafuu matokeo yake wanadhurika zaidi.
Ndio maana mimi huepuka kutoa ushauri wa aina yyt zaidi ya kumwambia mgonjwa akaonane na daktari.
Tuko pamoja .
 
Mkuu Tatizo sio yeye.
Tatizo liko kwenye hali ya maisha.
Watu wengi hapo Tz wanatafuta tiba nafuu matokeo yake wanadhurika zaidi.
Ndio maana mimi huepuka kutoa ushauri wa aina yyt zaidi ya kumwambia mgonjwa akaonane na daktari.
Tuko pamoja .

kumbe we huwa ni dokta kweli?!, huwa naona Ritz mzee wa kashata akikuita mi nadhani ni ule u dokta mwingine...
 
Last edited by a moderator:
kumbe we huwa ni dokta kweli?!, huwa naona Ritz mzee wa kashata akikuita mi nadhani ni ule u dokta mwingine...

U doctor mwingine ndio upi?
Au una maanisha km wa Slaa wa upako upako?
 
Last edited by a moderator:
Poleni na majukumu ndugu zangu.

Nina mdogo wangu wa kike umri ni miaka 20 ana tatizo la kuota vipele kama vichunusi kwenye miguu yake ambavyo hufikia muda vinaiva na kutoa usaha na vinaota kila siku anapojikuna kwan vinamwasha sana.

Kuna dawa ambayo alianza kuitumia kutoka kwa mhindi ya kupaka na ya kunywa ila hakuna mabadiliko zaid yameongezeka maumivu sana,ana wiki 2 toka aanze kuitumia iyo dawa.

Naomba mnisaidie wataaluma na Mungu awabariki.
 
Itakuwa kuna kitu aliwahi kula ambacho anaareji nacho hvyo vipimo vinahtajika
 
Mpeleke hospitali maana hata mimi nilishawahi kuvipata nikachoma sindano kwa siku saba ndio nikapona nakumbuka nilikuwa form 2
 
Kama imefikia pabaya ni kuwahi tu hospitali mapema siyo JF tena kiongozi...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…