Msaada tafadhari

matamba1

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2015
Posts
233
Reaction score
84
Habari za muda huu wana Bodi.
Naomba kujua angalau kwa undani kuhusu ugonjwa huu wa UTI hasa kwa kina dada,je ni ugonjwa wa zinaa?

stori nzima iko hivi....
Jana kaja rafiki yangu akiwa mnyonge zaidi ya vile nilivyomzoea nilipomuuliza akanisimulia "yeye na mpenzi wake wa muda mreefu wako kwenye mkwaluzano" wiki 3 nyuma mpenzi wake alienda kwa Dr kucheki afya akakutwa na UTI akaanzishiwa dose ya sindano lakini Dr akamshauri ampereke na mwezake jamaa alipoambiwa na garl wake hakua mbishi akaenda pale pale hsptl na girl wake majibu yalipotoka ikaonyesha yeye hana maambukizi hayo ya UTI,
Binti akamaliza dose lakini doctor alimkataza asifanye mapenzi na boi wake mpaka mwezi upite apimwe tena.
Sasa kinachomuumiza Rafiki yangu mpaka akaja kunisimulia ni Anahisi mpenzi wake sio muaminifu?
Naomba mwenye uelewa kidogo kuhusu haya matatizo ya UTI anielezee ili niweze kumpa hayo rafiki yangu maana naona anakuwa Amakufa moyo na kupoteza tumaini kwa mpenzi wake ampendae.
Ahsante...naomba kuwakilisha
 
Tatizo alilo nalo rafiki yako siyo unalolizungumzia ndugu, mwambie akueleze kweli alichoambiwa..

Kumbuka ugonjwa ni siri ya daktari na mgonjwa, huenda akakuficha au kukudanganya pia.
 
Tatizo alilo nalo rafiki yako siyo unalolizungumzia ndugu, mwambie akueleze kweli alichoambiwa..

Kumbuka ugonjwa ni siri ya daktari na mgonjwa, huenda akakuficha au kukudanganya pia.

Hapana ni rafiki yangu ambae huwa hatufichani kitu ndio maana akaweza kuniambia haya hata kuileta hapa ni ruhusa yake ili ajue.
 
Owkay,
Kwanza huu ugonjwa ni kweli unaambukiza kwa njia ya kujaamiana endapo mmoja kaathirika tayari, ila nikujibu kutokana na maelezo yako hapo.

Pili, hakuna uhusiano wa moja kwa moja kupata ugonjwa huo kwa njia moja tu ya kujaamiana, kwa sababu kuna njia nyingi na mojawapo ni hii hapa; Kutokana na mfumo wa maisha ya kisasa ambapo kila kitu ni UZUNGU, vyoo vingi tukienda kujisaidia hasa hv vya kisasa mara nyingi watu wanaingia kujisaidia kila mtu na maradhi yake hvo basi unaweza kujisaidia short call kwenye kile ki_beseni kumbe aliyetoka hapo haku_flash maji na ni muathirika na huo ugonjwa, so urine yako ikigongwa kwenye ukuta wa hicho kibeseni basi wadudu wanarukia kwako.

Tatu, hii Urinary Tract Infection mara nyingi inaathili sehemu ya njia ya mkojo, hivo basi hata vinywaji tunavokunywa hususani Maji, na Juice za majumbani ambazo waandaaji wake hawakufikia vigezo vya usafi, hivo wadudu hao jamii ya candida(kama sijakosea) na jamii ya fungi's hujiliwaza humo kusubiri waingie sehemu ya njia ya urine.

Ndiyo maana wale walio ambukizwa huu ugonjwa upata maumivu makali wakienda msalani kupata short call.
 

Hii ya pili inaweza kuwa sababu ya msingi sana maana jamaa hana afu girlfriend wake ana hilo tatizo.
mkuu itakuwa vema na ya tatu ukiimalizia kwani wengi watajifunza pia kupitia uzi huu
 
UTI-URINARY TRACT INFECTION,NI UGONJWA WA MAAMBUKIZO KWA NJIA YA MKOJO.UTI SIO STDs,ni ugonjwa wa kawaida unaotokana na matumizi wa vyoo vilivyo na maambukizo.
 
UTI-URINARY TRACT INFECTION,NI UGONJWA WA MAAMBUKIZO KWA NJIA YA MKOJO.UTI SIO STDs,ni ugonjwa wa kawaida unaotokana na matumizi wa vyoo vilivyo na maambukizo.

Ahsante mkuu naona hata TODYS kaifafanua vzr nadhani inaeleweka
 
By NEGLIGIBLE
Comrade naomba urekebishe jina uliloandika hapo kama ni langu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…