Msaada tatizo wakati wa tendo la ndoa

sparcus

Senior Member
Joined
Feb 18, 2014
Posts
193
Reaction score
125
Habari wana jamii, naombeni msaada wenu juu ya hili kwakweli sielewi ni nini hasa,
Mimi nna mpenzi wangu ambae nimekua nae kwenye mahusiano kwa muda wa mwaka na nusu sasa na tumeshiriki ngono sio chini ya mara kumi, tatizo lilipelekea kuomba msaada ni juu ya kilichotokea wakati wakufanya hilo tendo, ni mara ya pili sasa umenitokea nafanya nae mapenzi mzunguko wa kwanza unaisha vizuri, ila tukirudia anatoka damu hata kama nilimuandaa vizuri na yeye akahitaji nimuingilie,suala hili hunikatisha hamu kabisa yakuendelea kushiriki na jogoo wangu hukataa kabisa.
Na hata nikimuulia kama alikuwa amekaribia kuingia kwenye mzunguko wake wa mwezi hukataa na nikimuuliza kama amepata maumivu pia hukataa nashindwa kuelewa ni nini tatizo na tiba yake ni nini naombeni msaada wenu

Naombeni mnisaidie majibu ya kashfa au matusi sio mazuri hamtanisaidia mkifanya hvyo
Asanteni na karibuni kwa msaada
 
Asante mwa msaada #kisima
Ntafurah wakija nkapata msaada zaid

Hujambo kijana,

Jambo la kwanza nakushauri umfikishe mpenzi wako hospitali yenye mtaalamu wa magonjwa ya wanawake popote ulipo.

Pili kuna sababu kadhaa zipelekeazo mwanamke kutokwa na damu wakati wa tendo la ngono au baada ya kumaliza kufanya ngono.

1. Yeast Infection, maambukizi ya fangasi za uke huwa ni moja ya sababu zipelekeazo shida hii, kama uke wa huyo binti unatoa kitu mfano wa cheese nyeupe isiyo na harufu ni dalili kuwa huenda ana maambukizi ya fangasi.

2. Kukwaruzika kwa kuta za uke kunakotokana na ukavu wa uke

3. Endometriosis, hii huwa ni hali kama ya inflammation kwenye kuta za mji wa mimba, kiasi kwamba tishu za endometrial zinajitengeneza hadi nje ya mji wa mimba na mwishowe husababisha damu kidogo kutoka.

4. Ukuaji usio wa kawaida wa shingo ya kizazi, wakati mwingine shingo ya kizazi hutiririsha damu ikiwa ni dalili za awali za ukuaji wa seli za kansa.
Ukiachana na hili pia huwa kuna ukuaji mwingine uitwao polyps ambao wenyewe hauna uhusiano na kansa nao huweza kusababisha utokaji damu.

5. Magonjwa ya zinaa, kwa kuwa umeanza kushiriki zinaa hapa naamini unayajua magonjwa haya

6. Matumizi ya vidonge vya uzazi wa mpango; vidonge vya uzazi wa mpango huongeza kichocheo kiitwacho estrogen na ongezeko la kichocheo hiki husababisha shingo ya uzazi kushuka chini kidogo kuelekea vaginal opening.
Kutokana na ulaini wa tishu za shingo ya uzazi, kuna uwezekano wakati wa tendo la ngono kukawa na msuguano unaoweza kupelekea utokaji wa damu.

Mwisho,kwa faida yako acha uzinzi
 



Sijambo
Asante nashukuru kwa msaada,pia samahani naomba kufaham kama ana dalili hiyo ya kwanza uliyotaja yakutokwa na cheese nyeupe isiyo na harufu na kuwa na hizo fangas kuna uwezekano wakunipa maambukizi yoyote yale kiafya na pia zile damu zake kuna uwezekano wakunipa maambukizi pia kama sikushiriki tendo kwa kondomu
 

Maambukizi ya fangasi hutokea sana kwa wanawake kutokana na namna maumbile yao ya siri yalivyo.

Ingawaje mwanaume anaweza kupata aina hii ya maambukizi kama alishiriki ngono zembe na mwanamke mwenye yeast infection.

Hata hivyo chances za kupata maambukizi ni ndogo sana...
 
Umenikumbusha mbali kweli! Kuna binti flani ilikuwa the same, yaani hata asipoingia period siku hiyo basi kesho yake lazima aingie! Baadae sana hiyo hali ilipotea, nadhani ilikuwaga uoga wake tu! Manake anaweza ingia wiki hii, mkasema mko poa next week mkipiga gemu anaingia tena!
So possibly ni the same!
Note yy mzunguko wake ulikuwa hauko sawa, anaweza maliza hata miezi miwili bila ingia period
 



Asante sana #watu 8
Naweza faham mahali madaktari wa magonjwa ya wanawake wanapopatikana na je?, anaoenda kupima kuna ulazima wa mimi pia kupima pamoja nae ili kujua kama nmeambukizwa?
Na kuna uwezekano wa kukaa mda gani ili kujua kama umeambukizwa au la, na zipi dalili za maambukizi kwa mwanaume
 

Kuna uwezekano wa jambo hilo? Mbona ni wiki mbili tu tangu atoke period
Kuna sabab za kiafya zinazoweza kupelekea hili?
 
Kuna uwezekano wa jambo hilo? Mbona ni wiki mbili tu tangu atoke period
Kuna sabab za kiafya zinazoweza kupelekea hili?

Ndo hivo! Ni kweli tupu, mwanamke anaweza akawa labda na hofu either ya tendo au mimba na ikasababisha hiyo hali kujitokeza. Wanatofautiana sana!
 

Kama umenielewa vizuri tokea mwanzo, maambukizi ya fangasi huweza kusababisha tatizo hilo limpatalo huyo binti hivyo si lazima chanzo kikawa ni hicho.

Nenda hospitali yoyote ya serikali (kuanzia zile za wilaya, mkoa au rufaa) au hospitali binafsi kubwa, huko utapewa majibu yote ya maswali yako pamoja na vipimo stahiki.
 
inawezekana anatumia njia za uzazi wa mpango kuzuia mimba mfano vidonge au sindano
 
Samahani naomba kuuliza watu8
1.nilidhani vaginal yeast infection angekua na itchy sensation before even dyspareunia or post coital bleeding ingawa age hajasema but to my side dry vaginal mucosa as a cause ingekua high in the list with the least being cacx or bleeding cervical polyp.
2. Endometriosis after sex????? Kwa hili natia shaka, sijaona sehem yoyote inayosema kua clinical feature ni post coital bleeding and very likely angekua na dysmenorrhoea or irregular pv bleeding and mostly being cyclical.
3. STI as a cause of post coital pv bleeding?? Maybe ungetupa mfano cause we would expect more of dyspareunia or chronic pelvic pain.
 

Si mwendege HOSPITAL?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…