Msaada: Too much usingizi

Msaada: Too much usingizi

Mahondaw

JF-Expert Member
Joined
Apr 9, 2013
Posts
67,252
Reaction score
168,563
Habari zenu madaktari, manesi kwa wakunga wa jadi.

Takribani miezi kama miwili mitatu hivi nimekuwa nilisikia hali ya usingizi kupitiliza, naeza amka asubuhi nikajiandaa nikaenda kazini ..haipiti muda kazini natamani hata kutoroka nikalale.

Nikirudi kazini tu hata hamu ya kupika sina najisikia kulala tuu muda wote na hapo naweza lala wee kuanzia sa kumi jioni hadi Saa moja nkiamka najipikilisha kidogo nakula usingizi tena na nikilala sichukui hata muda Usingizi huooo kama umetumwa vile na nalala fofofo.Asubuhi sasa mpaka kuamka kasheshe yani najilazimisha tu mana nsipoamka ntakufa maskini na kulala njaa..

Weekend sasa balaa tupu ile nshakunywa chai tu usingizi...nalala weeeee mpaka basi .. nkiamka naeza jiangalizisha muvi kidogo muvi haijaisha najiskia kulala. Muda mwingi napokuwa idle yaleyale mpaka majirani wananishangaa na muda mwingine siku nzima sitoki nje nimelala tu nkitoka haaa we kumbe ulikuepo!!!??? eeeeh nipo!

Kama ni ujauzito sina mana juzi tu nmetoka kuuona month kama si moon!

Sasa nashindwa kuelewa nini hasa kimesababisha hali hii?? Je kuna ugonjwa wa usingizi? kama upo nini dawa yake???

Nawasilisha...!
 
ratiba yako ya siku ikoje(on average na muda halisi wa matukio).....huwa unakula nini....mazoezi unafanya?....hivi vinaweza kusaidia kugundua tatizo..
 
ratiba yako ya siku ikoje(on average na muda halisi wa matukio).....huwa unakula nini....mazoezi unafanya?....hivi vinaweza kusaidia kugundua tatizo..

asubuhi kazini, nkirudi itategemea kama nina tushughuli twa hapa na pale ..mazoezi sifanyi kabisa ila kazini ni mbali wastani sometimes naamua kutembea tu..kula ni kasheshe nkinywa chai sometimes mchana sili kuja kula jioniii au usiku chakula chenyewe nagusa gusa tu !
 
asubuhi kazini, nkirudi itategemea kama nina tushughuli twa hapa na pale ..mazoezi sifanyi kabisa ila kazini ni mbali wastani sometimes naamua kutembea tu..kula ni kasheshe nkinywa chai sometimes mchana sili kuja kula jioniii au usiku chakula chenyewe nagusa gusa tu !
hizi topic zinaweza kukusaidia kwa namna moja ama nyingine...
[h=1]Topic: Kulala sana ni ugonjwa?[/h]
[h=1]Topic: kulala kupita kiasi[/h]


cc:
MziziMkavu
https://www.jamiiforums.com/member.php?u=13422
 
hapana jamani nina kilo chini ya 55 eti!

ingia kwenye profile yangu uone picha yangu...nilikuwa na 50kg...nilipoanza kulala nimekuwa kama nguruwe nakwambia!karibu kwenye ulimwengu wa mabonge nyanya!!
 
ingia kwenye profile yangu uone picha yangu...nilikuwa na 50kg...nilipoanza kulala nimekuwa kama nguruwe nakwambia!karibu kwenye ulimwengu wa mabonge nyanya!!

hapana jamani mi mwili umegoma kabisa!
 
Have you ever heard about mold? Just google yourself for more information, kulala sana kuna uhusiano na kushuka kwa homoni zako especially cortisol! Ambayo watu wengi waliokuwa exposed na mold huwa nayo na pia inaonyesha huna hamu ya kula zote hizo ni dalili zake, as the time goes by utajikuta unakosa kufurahia maisha na matatizo ya mood na dalili nyingine nyingi, jaribu kufanya uchunguzi wapi kuna growth ya mold aidha nyumbani au ofisini.
 
Fanya mazoezi,penda kunywa maji mengi,usioverload kazi au shuhuli za siku.
 
Aisee si unipe mimi huo usingizi maana mi sipati usingizi kabisa nalala saa nane au tisa usiku kila siku tena kwa kujilazimisha na nikifika kitandani ni shida kusinzia. Na nikiupata akipita mtu yaani ata ajikune tu lazima nishtuke.
 
Back
Top Bottom