Msaada tutani: Mwenye mkataba wa biashara ya Bodaboda

tramadol

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2015
Posts
5,383
Reaction score
4,323
Wadau habarini,

Kuna ndugu anahitaji kununua pikipiki kwa ajili ya biashara na ni mara ya kwanza kufanya hiyo biashara lakini katika uchunguzi wake amegundua kuna aina tatu ndani ya biashara ya bodaboda

Kwanza ni mwenye bodaboda kuendesha mwenyewe pikipiki kibiashara

Pili kuna mkataba wa mwenye pikipiki na dereva wa bodaboda kwa kukusanya mauzo kwa wiki na dereva kumpa mwenye pikipiki bila muda maalum kama vile daladala kupeleka hesabu kwa mmiliki

Tatu kuna mkataba wa muda maalum wa malipo kwa mwenye pikipiki na dereva na baada ya muda huo wa malipo kukamilika then pikipiki unabadilishwa umiliki na kukabidhiwa dereva moj kwa moja

Sasa maombi kwenu ni kupata mkataba huu wa tatu yaani muda maalumu wa malipo then pikipiki inabadilishwa umiliki wake baada ya muda huo

Nashukuru kwa ushirikiano wenu wadau
 
Sema tu kwamba ni wewe mwenywe ndio mwenye shida ya huo mkataba na sio ndugu yako. Wanajf wengi mkija humu na tatizo au shida huwa mnakuja na "gia" ya ndugu yangu ndio anashida au jamaa yangu.
Ok,kwa kukusaidia tu tafuta wakili mpe hiyo kazi nae apate "ulaji" kidogo akushughulikie swala lako.
 
Kama upo Dar njoo PM haraka ili tupange wapi tuonane ili uichukue hiyo mikataba mkuu.
 
Na vipi kama kweli ni ndugu yake kweli anahitaji msaada?
 
nliacha boda nikanunua bajaj guta nayo vurugu tupu nipo nimeitunza home naitumia mwenyewe kwa shughuli ndogondogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…