Msaada, naomba kujuwa yafuatayo;
1. std size ya nyumba ya kisasa
2. std size ya Master
3. std size ya public toilet
4. std size ya sitingroom na dining, kitchen.
Nb. nataka nyumba ya vyumba 2 na master1, public toilet n shower, dining, kitchen, store, sitting room.
Asante
Mkuu BwanaX kuna mambo mengi ya kuangalia wakati wa ku-design nyumba nitajaribu kuelezea machache kabla sijajibu swala lako.
a) Taste ya mtu...
Pamoja na kwamba kuna standards kama guide lakn bado taste ya mtu ni input mhimu wakati wa ku-design. Mfano mwingine anataka jakuzi kwa bathroom,mwingine hataki, mwingine anataka bedroom ziwe na vitanda viwili vivili, makabati(wadrobes)...n.k n.k
b) Uelekeo wa upepo (wind direction)...
Hii inaleta dhana ya kuamua mashimo ya choo (septic tank na soakaway pit) yakae sehemu gani ya nyumba(vyovyote iwavyo si vizuri kuyaweka mbele ya nyumba)
c) Uelekeo wa jua...
Hii inaleta dhana ya orientation ya nyumba, mara nyingi si vizuri kuweka vyumba vya kulala jua linakozamia, especially master bedroom, ili unapoenda kulala usikute joto liko juu
d) Size ya kiwanja...
Size ya nyumba ni function ya size ya kiwanja, haiwezekani kwa sababu unataka nyumba ya size flani basi ujenge nyumba inayo-cover kiwanja chote bila hata ya kuacha nafasi ya watoto kucheza, it must be designed to well fit in the plot.
e) Functional design/Requirement. ...hapa tunazungumzia uhusiano wa vyumba (connectivity), mfano jiko, dining na lounge havipaswi kuwa mbali mbali sana, na hapa ndipo tunapokuta PRIVATE AREA NA PUBLIC AREA, principally haya maeneo mawili yanapaswa kuwa distinct, yaani akija mtu ambae si sehemu ya familia hatakiwi ajue kirahisi vyumba vya kulala viko wapi na vikoje. Katika ku-fulfil hii requirement inaathiri size ya nyumba.
f) Spacial design/requirement
Sehemu hii designer anajaribu kutumia elimu yake kwa kutumia standards(ulizoulizia) pamoja na taste za mteja ili kupata size za vyumba mbalimbali na hivyo kupata size ya nyumba.
Binafsi ningeshauri nyumba iwe na vyumba vyenye range ya size zifuatazo, size ni katika square metre(sqm)
1.Master bedroom.....14 - 25 plus bathroom/toilet.....3 - 4
2. Bedroom....9 - 14, if is self contained add bathroom/toilet...2.4-3
3. Public toilet. ...2.4 - 3
4. Sitting room. ...22.5 - 36
5. Dining room. ...7.5 - 12
6. Kitchen. ....9 - 16
7. Store....3 - 4.5
Ushauri
Kwa kuwa ujenzi unagharimu fedha nyingi ni busara kupata design nzuri kutoka kwa wataalam hata kama hutatumia wataalam wakati wa ujenzi kuepusha kujilaumu baadae. Ni vizuri pia kujenga katika kiwanja kilichopimwa.