Msaada: Upatikanaji wa vifaranga wa mayai

Msaada: Upatikanaji wa vifaranga wa mayai

chan lee

Senior Member
Joined
Jun 30, 2013
Posts
149
Reaction score
41
Habari wakuu..! Msaada hapo juu ya bei na mahali nitakapoweza kupata vifaranga vya mayai...!
Natanguliza shukran..!
 
Nenda TAZARA kwenye mataa uelekeo wa Uwanja wa Taifa, kuna Jamaa amenielekeza kwamba pale wanauzwa....
 
Poa poa mkuu..! Thanx much...!@TANMO
 
Kwa hawa kuku wa kisasa ni bora ununue kwa makampuni yenyewe au kwa wakala wao hapo Tazara ni madalali hawafai kwa uzoefu tu wanawauzia watu vijogoo au hawa wa kienyeji na utapata hasara, pia vifaranga vyao mara nyingine wazazi hawakupewa chanjo hivyo vifo huwa vingi na huna wa kumlaumu maana ukirudi hukuti mtu. Nenda ubungo mataa pale wanauza wa Mkuza Farm, Interchick au agent wao mabibo opposite na EPZA ulizia hao watakuelekeza. Pia Kenchick wana magari yao yanapaki kila jumanne na Alhamisi nyuma ya YMCA na kuuza vifaranga njoo uulizie. Vifaranga wa kisasa ni bei na kuwalisha gharama ukiuziwa feki ni hasara sana.
 
Kwa hawa kuku wa kisasa ni bora ununue kwa makampuni yenyewe au kwa wakala wao hapo Tazara ni madalali hawafai kwa uzoefu tu wanawauzia watu vijogoo au hawa wa kienyeji na utapata hasara, pia vifaranga vyao mara nyingine wazazi hawakupewa chanjo hivyo vifo huwa vingi na huna wa kumlaumu maana ukirudi hukuti mtu. Nenda ubungo mataa pale wanauza wa Mkuza Farm, Interchick au agent wao mabibo opposite na EPZA ulizia hao watakuelekeza. Pia Kenchick wana magari yao yanapaki kila jumanne na Alhamisi nyuma ya YMCA na kuuza vifaranga njoo uulizie. Vifaranga wa kisasa ni bei na kuwalisha gharama ukiuziwa feki ni hasara sana.

Asante Mdau, umenifungua macho manake nilielekezwa tu bahati nzuri nilikuwa sijakwenda pale..
CC: chan lee
 
Back
Top Bottom