Kisonono ni
maradhi ya zinaa ambayo husababishwa na
bakteria zinazofahamika kisayansi kama
Neisseria gonorrhoeae. Bakteria hizo hushambulia utandotelezi unaozunguka
sehemu za siri.
Ingawa kwa makisio maambukizi 360,000 ya kisonono huripotiwa kila mwaka nchini
Marekani, wataalamu wamekisia kuwa watu karibia 650,000 huambukizwa kwa mwaka.
Kama ilivyo
klamidia, kisonono nayo huwa haionyeshi
dalili. Kisonono ikiwepo huwa na dalili kama zile za
klamidia ambazo huhusisha mauvimu wakati wa kukojoa na kutokwa kwa
maji yanayonuka au
usaha katika
uke au
uume.
Kisonono huonekana kwa urahisi kwa wanaume ambao hutoa
usaha kutoka katika mfereji wa mkojo (
urethra). Huanza kidogo, lakini huongezeka na huwa mwingi na kusababisha kusikia haja ya kukojoa mara kwa mara huku kukiwa na maumivu.
Kisonono ikisambaa na kufikia
prostate, mfereji wa mkojo huziba kwa kiasi fulani. Kwa wanawake maambuki hutokea katika
urethra,
uke au
mlango wa uzazi (
cervix). Ingawa mwasho unaotokana na majimaji katika uke unaweza kuwa mkubwa, mara nyingi dalili hizi huwa ni chache au hamna kabisa katika hatua za awali.
Kisonono isiyotibiwa inaweza kusababisha PID kwa wanawake. Watoto wanaozaliwa na mama wenye kisonono huwa na hatari ya kuambukizwa wakati wa kuzaliwa; maambukizo haya yanaweza kusababisha magonjwa ya
meno kwa wachanga.
Uchunguzi wa ugonjwa hufanywa kwa kuchungunza usaha kutoka katika uke au uume au mkojo kwa uwepo wa
Neisseria gonorrhoeae.
Kisonono iliongezeka kwa kiasi kikubwa
Marekani mnamo miaka ya
1970 na mwanzoni mwa miaka ya
1980, hadi kukaribia kufikia kiwango cha
magonjwa ya mlipuko (
epidemic proportions) kwa vijana wanaobalehe na watu wa
umri wa kati.
Kisonono hutibiwa kwa
antibaotiki kadhaa, ingawa maambukizi yamekuwa na ukinzani juu ya tiba ya baadhi ya madawa katika miongo ya nyuma. Moja kati ya mambo magumu katika kupambana na
kisonono ni kutafuta mahusiano yote ya kimapenzi ya nyuma ya aliyeambukizwa ili kuweza kuzuia usambaaji zaidi wa ugonjwa.
Ushauri wangu nenda Haraka Hospitali kujiibia huo ugonjwa Mkuu.@