Kuna dada mmoja anasumbuliwa sana na tatizo la kupata maumivu
makali anapokuwa kwenye menstruation (dysmenorrhoea), jambo
linalomnyima raha. Amejaribu sana tiba za hospitali bila mafanikio
na alishauriwa kuwa asubiri atakapopata mtoto tatizo litakwisha.
Tulikuwa katika maongezi ya kawaida tu akagusia jambo hilo kwetu.
Kama kuna yeyote anayejua kuhusu tiba ya tatizo hili anijuze ili
nimsaidie...