Habari za kazi wadau? Mimi ni kijana ambaye nimeajiriwa katika mkoa wa Singida, mbali na kuajiriwa nimeona kuna fursa ya kufanya biashara ya kununua asali kwa wafugaji wadogo na kuifunga katika chupa za lita moja na nusu lita, na sasa nimefikia hatua ya kukopesheka katika taasisi moja ya mikopo hapa Singida, na mimi nategemea mshahara wangu katika kufanya hayo marejesho kwa sasa, jambo ambalo linanichanganya ni muda wa kupokea mshahara hautabiriki na itakuwaje kama nikiacha kazi jinsi ya kurejesha huo mkopo? Nawasilisha