huo ni mchakamchaka!!
mwanangu alikataa kunyonya akiwa na miezi 2. Nilikomajee!!! Kila nikimpa maziwa ya kopo anaharisha...
kakuzwa na maziwa ya ng'ombe tu mpk akipofikisha miezi 5 ndipo nilipoanza kumpa uji wa dona, alipoanza wa 7 nikaanza kumpa uji wa lishe niliopikia maziwa bila kuacha maziwa na vijuice kimtindo! viugali kwa mbali, mara vimtori, mara visupu vya samaki, na mbogamboga, jana katimiza miezi 8 ana kilo za kutosha kbs, anaafya nzuri na anavutia machoni pa watu.
Namshukuru Mungu hajawahi kuugua kivile japo waliniambia mtoto ambae hajanyonya ni hekalu la magonjwa.
Nimejifunza mengi kupitia mitandao, jinsi ya kumtengenezea chakula, jinsi ya kumtengenezea uji wake wa lishe,kumlisha matunda na vitu vingi.
leo naitwa mama Bonge.