Msaada wa kimawazo katika hili

Mimi mwezi ulopita hapo nimenunua $ kwa 2599 (BOT) 😀😀😀 Mpaka kichwa kilidata,Nilipokuwa nafanya T.T.​
 
Wanakureport wapi kwa mfano? Yaani wakulazimishe kununua gari kwa pesa yako?
 
Imetumwa leo,nahisi wataireport account yangu kwamba ni tapeli.
Hamnaga kitu kama hicho. Nimeshapitia hiyo situation mara zaidi ya 10. Cha msingi unawasiliana na muuzaji na unamwambia sababu ya kuchelewa kufanya malipo.

Hiyo deadline aliyokupa ya tarehe ni deadline ya kimasoko kwamba hadi kufikia hiyo tarehe ukiwa haujalipia hiyo gari then wairudishe kule kwenye website ili wanunuzi wengine waweze kuilipia na kuchukua.

Na ndio maana akiwa amekutumia invoice kule gari utaona picha imeandikwa kuwa gari ipo under negotiations na mteja inawezekana kununuliwa ila inabakia kuwapo katika display ya picha za kwenye website.
 
Hapana,wamenitumia message hii,please note we might suspend your account if you do not pay your order by the due date.
Hamnaga hiyo kitu, kampuni gani hiyo wamekutumia vitisho namna hiyo?

Au huwa unakwenda kuzuia gari unaomba proforma invoice halafu haununui?
 
Hakuna kitu kama hicho

Mimi nmeagiza gari miezi miwili iliyopita SBT

Hakuna sehemu nlifosiwa kulipa,
Wao usipolipa wanarudisha gari sokoni basi

Ni kampuni gani iyo??

Nashauri usifanye haraka kulipa!!!!!!

Jiridhishe upya!!!
Huyu au ameagiza gari Instagram?
 
Hamnaga hiyo kitu, kampuni gani hiyo wamekutumia vitisho namna hiyo?

Au huwa unakwenda kuzuia gari unaomba proforma invoice halafu haununui?
Ndo mara ya kwanza sijawahi.Real motor japan hao.leo nimewajulisha sitaweza kufanya malipo nimekosa dollar.
 
Achana nao faster
 
Ndo mara ya kwanza sijawahi.Real motor japan hao.leo nimewajulisha sitaweza kufanya malipo nimekosa dollar.
Agizia na kampuni zenye reputation kama Befoward, Autocom Japan, SBT hawa wanaweza kukupa option nyingi sana hata ukiwa na hela nusu gari wanakupakizia kwenye meli salio unakuja malizia gari ikiwa inakaribia kufika au ikishafika bandari kabla haujapewa karatasi zake kwaajiri ya kuiprocess.
 

Ukifata huu ushauri tunafunga thread tujadili mambo mengine
 
Hao waliokupa vitisho ninahisi ni matapeli. Kuna wakati website ya Real Motor, ukifungua kupitia Google Chrome, ilikuwa inaonesha security yake si salama. It wasn't safe. Huenda kuna matapeli wameikamata.

Beforward yes wana akaunti ya kulipa kwa shilingi. Hakunaga vitisho kwenye biashara ya mtandaoni. Kwani ugomvi nisiponunua kwao? Nenda kwenye ofisi za Beforward ukaagize ndinga nyingine.
 
Hapana,wamenitumia message hii,please note we might suspend your account if you do not pay your order by the due date.
Sasa hawa wao ndo matapeli hakunaga biashara yenye lugha mbovu na kutishana kifala ivo, na hata ukiona vipi temana nao, tafuta gari kwa makampuni mengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…