Kapepo
JF-Expert Member
- Aug 14, 2015
- 1,066
- 1,194
Kwa kifupi ni kwamba kuna vishilingi veupe ambavyo huongezeka ukubwa lakini haviumi , vinanitoka mara kwa mara upande wa kulia wa kinywa changu, nimeenda hospital nimetumia dawa nyingi tu lkn huja na kutoweka vyenyewe. Pia nasumbuliwa na kiungulia cha kawaida kwenye tumbo hadi kwenye kifua, kuhisi kama kuna mabaki ya chakula kwenye kinywa nyuma ya ulimi, lips kuwa zimepauka, kuhisi kama nimekula pilipili kwenye lips na maumivu kwa mbaali sana kwenye koo pamoja na masikio kuuma kwa mbali mara nyingine kuwasha, vile vile niamkapo asubuh napiga chafya sana. Kilichonitisha zaidi leo asubuh nimeamka nimekuta kidoti cheusi pembeni ya ulimi upande wa kushoto lkn baada ya kupiga mswaki kimepotea lakn eneo hilo lina maumivu tena kwa mbali sana Naombeni ushauri wenu wakuu.