Alan Madiga
Member
- Apr 28, 2013
- 26
- 2
WanaJF, nimeishi kwa miaka ishirini na sita (26) sasa nikiwa nimepoa moyo kabisa. Sina hisia za upendo na sijawahi kuhisi hivyo toka mwaka 1996 nilipokuwa darasa la pili.
Nakumbuka mwaka huo nilikuwa darasa la pili na tulikuwa tunaishi kota, enzi zile shule tulikuwa tunatoka saa nne asubuhi.
Nyumbani nilikuwa nashinda na mfanyakazi wa kike wa jirani yetu.
Huyo mdada alikuwa ni mtu mzima tayari na alikuwa akinifanya mimi kama mpenzi wake. Kwa umri niliokuwa ilikuwa ngumu kujua kama nilikuwa nabakwa wakati huo na nilitumika kumridhisha huyo binti pasi na kujua lolote.
Haikuishia hapo kuna likizo moja mimi na mama yangu tulikwenda kumtembelea bibi kijijini. Huko ilinitokea hali hiyo ya kutumiwa kimapenzi na mama yangu mdogo. Hii iliniumiza sana kuujua utupu wa mama yangu mdogo nikiwa bado mdogo sana na sikujua ananitendea jambo gani.
Sasa nimepevuka na najua mema kwa mabaya. Nilijaribu wakati ule kusema lakini hakuna aliyekuwa tayari kunisililiza vile wazazi walikuwa bize na shughuli zao.
Ili nijengea hali ya uoga na kutojiamini mbele za watu hivyo ikanifanya nianze kujitenga na kuwa mbinafsi kadri ninavyokua.
Hakuna aliyejali kuhusu mimi kwa nini mimi nijali kuhusu wao?
Nilipo barehe na kuanza mahusiano ya kimapenzi na wasichana, kuna hali ya roho ya ukatili na kisasi inanitawala mpaka nashindwa kudumu na msichana yoyote yule.
Naona hakuna binadamu mwenye kujali shida za mwingine zaidi ya kila mtu kujali kutimiziwa haja zake tu. Nimejitumikisha ktk hali ya kulipa kisasi na kujiridhisha nafsi yangu kwa zaidi ya miaka 15 lakini bado sijaweza kupata ahueni ya kisaikolojia ili nisahau vitendo vya kubakwa utotoni.
Nimewaumiza wengi na sasa nimechoka na nahitaji msaada wa matibabu ya kisaikolojia ili niweze kupenda km wengine wanavyopenda ndugu, jamaa, marafiki, wapenzi na maisha.
Nawakilisha.
Nakumbuka mwaka huo nilikuwa darasa la pili na tulikuwa tunaishi kota, enzi zile shule tulikuwa tunatoka saa nne asubuhi.
Nyumbani nilikuwa nashinda na mfanyakazi wa kike wa jirani yetu.
Huyo mdada alikuwa ni mtu mzima tayari na alikuwa akinifanya mimi kama mpenzi wake. Kwa umri niliokuwa ilikuwa ngumu kujua kama nilikuwa nabakwa wakati huo na nilitumika kumridhisha huyo binti pasi na kujua lolote.
Haikuishia hapo kuna likizo moja mimi na mama yangu tulikwenda kumtembelea bibi kijijini. Huko ilinitokea hali hiyo ya kutumiwa kimapenzi na mama yangu mdogo. Hii iliniumiza sana kuujua utupu wa mama yangu mdogo nikiwa bado mdogo sana na sikujua ananitendea jambo gani.
Sasa nimepevuka na najua mema kwa mabaya. Nilijaribu wakati ule kusema lakini hakuna aliyekuwa tayari kunisililiza vile wazazi walikuwa bize na shughuli zao.
Ili nijengea hali ya uoga na kutojiamini mbele za watu hivyo ikanifanya nianze kujitenga na kuwa mbinafsi kadri ninavyokua.
Hakuna aliyejali kuhusu mimi kwa nini mimi nijali kuhusu wao?
Nilipo barehe na kuanza mahusiano ya kimapenzi na wasichana, kuna hali ya roho ya ukatili na kisasi inanitawala mpaka nashindwa kudumu na msichana yoyote yule.
Naona hakuna binadamu mwenye kujali shida za mwingine zaidi ya kila mtu kujali kutimiziwa haja zake tu. Nimejitumikisha ktk hali ya kulipa kisasi na kujiridhisha nafsi yangu kwa zaidi ya miaka 15 lakini bado sijaweza kupata ahueni ya kisaikolojia ili nisahau vitendo vya kubakwa utotoni.
Nimewaumiza wengi na sasa nimechoka na nahitaji msaada wa matibabu ya kisaikolojia ili niweze kupenda km wengine wanavyopenda ndugu, jamaa, marafiki, wapenzi na maisha.
Nawakilisha.