Msaada wa kisheria kuhusu haya mauziano ya ardhi

Msaada wa kisheria kuhusu haya mauziano ya ardhi

masaho

Member
Joined
Apr 29, 2014
Posts
9
Reaction score
3
Nimenunua eneo la ardhi, aliyeniudhia hilo eneo ni mwanaume mbele ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa , kabla ya mauziano hayo niliulizia kuhusu umiliki wa eneo nikadhibitishiwa kuwa ni lake na nikahoji kama ana mke akasema hana mke walikwisha achana zaidi ya mwaka mmoja na walizaa mtoto mmoja na huyo mtoto yuko naye yeye anamlea.

Huyo mwanamke hakumuoa kwa ndoa waliishi tu na maelezo haya niliyathibitisha kwa balozi na majirani hivyo nikaridhika tukasaini hati ya mauziano.
Lakini ndani ya mwezi mmoja tokea tumeuziana kwenye hilo eneo akaingia mwanamke kuishi kwenda kumuuliza anasema yeye ni mke wa aliyekuuzia hili eneo wakati anakuuzia mimi hakunishirikisha hivyo sitambui uuzwaji wa eneo hili na akiwa na yule mtoto.

Hebu wanajamvi naomba msaada hapo kisheria
 
Pole sana kwa matatizo.kesi yako ni ngumu ila huo mkataba ulioingizwa utakuwa batili kama tu hiko kiwanja walikipata wakati akiishi na mke wake na waliishi zaidi ya miaka miwili hata kama hawakufunga ndoa sheria inatambua kuwa ni mke wake hivyo ilitakiwa ridhaa ya watu wote wawili wanandoa hao katika uuzaji huo.haya ni kwa mujibu wa sheria ya ardhi s. 67.na sheria ya ndoa s.160,58-60.kumbuka muuzaji wa ardhi lazima atoe maelezo yote muhimu yanayohusu uuzaji wa kiwanja na kiwanja lazima kiwe chake.
 
Asante bwana Alphred kwa ufafanuzi wako sasa ile pesa niliyoitoa sitoweza kuipata tena? maana yule aliyeniuzia kakimbia na hajulikani alipo kwa hiyo yupo tu mwanamke kwenye hiyo nyumba
 
Nenda kituo cha polisi kafungue complaint kuhusu huyo bw. aliyekuuzia pamoja na huyo kiongozi wa mtaa aliyejidai kufahamu kuwa eneo ni la muuzaji wakati ukweli anaujua. watafunguliwa kesi ya wizi wa kuaminika. alternatively kama vipi ongea na huyo mke mpe nusu ya bei uliyompa mume wake then akuachie kiwanja/nyumba. Hakikisha mnaandikishana.

Vinginevyo itakuwa imekula kwako.
 
Back
Top Bottom