Msaada wa kisheria kuhusu mtu kuweka number kwenye mitandao bila ruksa

apollo jr

Member
Joined
Sep 3, 2015
Posts
48
Reaction score
36
naomba msaada wana jamvini, sheria inawezaje kumhukumu mtu ambaye bila ya ruksa kaweka number ya msichana mmoja kwenye mitandao na kudai kwamba eti anatafuta mchumba, wakati siyo kweli... sasa usumbufu mkubwa wakupigiwa simu anaupata huyu dada naombeni msaada
 
Wanasheria hutawakuta humu...hawapitagi sijui

Ila mmejaribu kitengo cha cyber bullying???
 
Mosi,
huyo amevunja haki yako ya faragha.(Right to privacy)
Katiba ya Tanzania katika Ibara ya 16 (1) inasema
"Kila mtu anastahili kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa nafsi yake, maisha yake binafsi na familia yake na unyumba wake, na pia heshima na hifadhi ya maskani yake na mawasiliano yake ya binafsi"


Pili,
amejifanya ni mtu mwingine kwa kupitia kompyuta.(Impersonation)
Hili ni kosa la kimtandao na adhabu yake ni milioni tano au miaka saba.

Ushauri wangu.
Mfuate muonye, akiendelea kukusumbua nenda polisi fungua jarada.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…