Msaada wa kisheria kuhusu swala la ndoa

Msaada wa kisheria kuhusu swala la ndoa

Emmado

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2010
Posts
225
Reaction score
276
Ndugu wadau!

Kuna mwanamke mmoja nilishawahi kuwa nae kimapenzi na baadae bahati akapata mimba, tukapata mtoto mmoja. nikajaribu kumweka ndani awe mke wangu, tulikaa miaka miwili pamoja, alikua na matatizo madogo madogo ya kitabia nikajaribu kurekebisha ikawa tabu ilipofika mwaka wa tatu mwishoni akaniambia amenichoka akaondoka na kila kilichokuwa chake.
Nilimbembeleza sana afikirie mara mbili ikashindikana, nikamshauri aniachie mtoto nimsomeshe akagoma ila baadae nikampeleka ustawi wa jamii ikaamuliwa anipe mtoto kwa ajili ya shule.

Tangia hapo nikawa nimepumzika rasmi kwa miaka mitatu, sasa tatizo limekuja juzi baada ya kusikia nataka kuoa akaanza kunitumia sms za ajabu ajabu ila ya mwisho akaniambia hawezi kuniacha nikaoa labda afe.

Sina tatizo sana na vitisho vyake ila;-
1} Je endapo akiamua kuja kuzuia ndoa yangu kwa pingamizi je atakuwa na nguvu kisheria
2] Naweza pata kinga ya kisheria ili hili lisitokee?
3] Nifanyeje asiniharibie tukio langu la kihistoria?


Naombeni msaada wadau!
 
Ndugu wadau!

Kuna mwanamke mmoja nilishawahi kuwa nae kimapenzi na baadae bahati akapata mimba, tukapata mtoto mmoja. nikajaribu kumweka ndani awe mke wangu, tulikaa miaka miwili pamoja, alikua na matatizo madogo madogo ya kitabia nikajaribu kurekebisha ikawa tabu ilipofika mwaka wa tatu mwishoni akaniambia amenichoka akaondoka na kila kilichokuwa chake.
Nilimbembeleza sana afikirie mara mbili ikashindikana, nikamshauri aniachie mtoto nimsomeshe akagoma ila baadae nikampeleka ustawi wa jamii ikaamuliwa anipe mtoto kwa ajili ya shule.

Tangia hapo nikawa nimepumzika rasmi kwa miaka mitatu, sasa tatizo limekuja juzi baada ya kusikia nataka kuoa akaanza kunitumia sms za ajabu ajabu ila ya mwisho akaniambia hawezi kuniacha nikaoa labda afe.

Sina tatizo sana na vitisho vyake ila;-
1} Je endapo akiamua kuja kuzuia ndoa yangu kwa pingamizi je atakuwa na nguvu kisheria
2] Naweza pata kinga ya kisheria ili hili lisitokee?
3] Nifanyeje asiniharibie tukio langu la kihistoria?


Naombeni msaada wadau!
akiamua kuja kuzuia ndoa yako kwa pingamizi, hana haki kisheria. hatakuwa na sababu yeyote kisheria kuzuia ndoa yako. kuhusu kinga ya kisheria, hilo naomba niwaachie wenzangu wakujibu ila huyo dada atakapoleta pingamizi kwa registrar au wakala wake kwenye zile siku 21 za tangazo nafikiri hatakuwa na sababu za kusilikizwa kama maelezo uliyoyatoa ni ya kweli. akija kujifanya anapinga baada ya siku 21 yaani pale kanisani au eneo la kufungia ndoa siku ile ya ndoa yenyewe huyo atakuwa mleta fujo tu na si mleta pingamizi kwasababu kuna siku 21 za pingamizi zimepangwa kwaajili yake na wenzake wengine kama wapo kuja kuleta pingamizi lao kama lipo. kama la msingi litasikilizwa kama si la msingi halitasikilizwa.

cha muhimu nafikiri, unatakiwa kumweleza huyo unayefunga nanye ndoa sasahivi ukweli wote uwe wazi asishitukizwe kwa chochote, ili hata siku akileta fujo huyo uliyezaa naye asipaniki na kuharibu mambo. uwazi ni kitu cha muhimu. nitakuwekea sheria ya ndoa hapa chini ili uidownload uisome. imeandikwa kwa kiingereza. pia nitakuwekea na link nyingine utakapopata sheria zilizoandikwa kwa kiswahili fasaha kabisa na sheria ya ndoa ipo huko pia.

bofya law of marriage Act bofya hapa View attachment SHERIA YA NDOA.pdf

kwa lini bofya hapa SHERIA KWA KISWAHILI
 
soma kifungu cha 160 cha sheria ya ndoa (pressumption of marriage)
 
akiamua kuja kuzuia ndoa yako kwa pingamizi, hana haki kisheria. Hatakuwa na sababu yeyote kisheria kuzuia ndoa yako. Kuhusu kinga ya kisheria, hilo naomba niwaachie wenzangu wakujibu ila huyo dada atakapoleta pingamizi kwa registrar au wakala wake kwenye zile siku 21 za tangazo nafikiri hatakuwa na sababu za kusilikizwa kama maelezo uliyoyatoa ni ya kweli. Akija kujifanya anapinga baada ya siku 21 yaani pale kanisani au eneo la kufungia ndoa siku ile ya ndoa yenyewe huyo atakuwa mleta fujo tu na si mleta pingamizi kwasababu kuna siku 21 za pingamizi zimepangwa kwaajili yake na wenzake wengine kama wapo kuja kuleta pingamizi lao kama lipo. Kama la msingi litasikilizwa kama si la msingi halitasikilizwa.

Cha muhimu nafikiri, unatakiwa kumweleza huyo unayefunga nanye ndoa sasahivi ukweli wote uwe wazi asishitukizwe kwa chochote, ili hata siku akileta fujo huyo uliyezaa naye asipaniki na kuharibu mambo. Uwazi ni kitu cha muhimu. Nitakuwekea sheria ya ndoa hapa chini ili uidownload uisome. Imeandikwa kwa kiingereza. Pia nitakuwekea na link nyingine utakapopata sheria zilizoandikwa kwa kiswahili fasaha kabisa na sheria ya ndoa ipo huko pia.

Bofya law of marriage act bofya hapa View attachment 147032

kwa lini bofya hapa sheria kwa kiswahili
​asante sana mungu akubariki sana!
 
Wakuu nameless girl na IDUNDA,mko sahihi. Pingamizi la kihalali kuhusu kufungwa kwa ndoa ni kuwepo kwa ndoa tu. Lakini,hii inategemea aina ya ndoa ambayo ilishafungwa hapo mwanzo.Kama ni ndoa ya wake wengi,bado mume aweza kuoa tena hata kama mke atapinga.Kwa ndoa ya mke mmoja,uwepo wa ndoa tu ni pingamizi tosha.

Mkuu Amavubi, kifungu cha 160 cha Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971, kinatoa nafasi kwa mwanamke aliyekaa na mwanaume kwa miaka miwili au zaidi kama mke na mume kupata chochote kutoka katika machumo iwapo mahusiano yao yatavunjika kutokana na kuhitilafiana. Hatahivyo, kifungu hiki hakitengenezi pingamizi kaika kufunga ndoa kama anavyotaka kufanya Mkuu Emmado.

Kwa ufafanuzi huu, Mkuu Emmado, waweza kuoa na huyu binti uliyezaa naye hawezi kuweka pingamizi la kisheria iwapo tu hukuwahi kufunga naye ndoa ya mke mmoja. Mwisho mwishoni, nitumie haki yangu ya ada ya ushauri kabla sijaweka pingamizi ha ha ha ha ha ha ha ha haaaaaaaaaaaaaaaa enjoy Mkuu!
 
Wakuu nameless girl na IDUNDA,mko sahihi. Pingamizi la kihalali kuhusu kufungwa kwa ndoa ni kuwepo kwa ndoa tu. OLakini,hii inategemea aina ya ndoa ambayo ilishafungwa hapo mwanzo.Kama ni ndoa ya wake wengi,bado mume aweza kuoa tena hata kama mke atapinga.Kwa ndoa ya mke mmoja,uwepo wa ndoa tu ni pingamizi tosha.

Mkuu Amavubi, kifungu cha 160 cha Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971, kinatoa nafasi kwa mwanamke aliyekaa na mwanaume kwa miaka miwili au zaidi kama mke na mume kupata chochote kutoka katika machumo iwapo mahusiano yao yatavunjika kutokana na kuhitilafiana. Hatahivyo, kifungu hiki hakitengenezi pingamizi kaika kufunga ndoa kama anavyotaka kufanya Mkuu Emmado.

Kwa ufafanuzi huu, Mkuu Emmado, waweza kuoa na huyu binti uliyezaa naye hawezi kuweka pingamizi la kisheria iwapo tu hukuwahi kufunga naye ndoa ya mke mmoja. Mwisho mwishoni, nitumie haki yangu ya ada ya ushauri kabla sijaweka pingamizi ha ha ha ha ha ha ha ha haaaaaaaaaaaaaaaa enjoy Mkuu!

Asante sana kiongozi.. Mungu Akubariki upate mara dufu ya ulichonacho leo
 
niseme tu kwamba every case has its own merits
Wakuu nameless girl na IDUNDA,mko sahihi. Pingamizi la kihalali kuhusu kufungwa kwa ndoa ni kuwepo kwa ndoa tu. Lakini,hii inategemea aina ya ndoa ambayo ilishafungwa hapo mwanzo.Kama ni ndoa ya wake wengi,bado mume aweza kuoa tena hata kama mke atapinga.Kwa ndoa ya mke mmoja,uwepo wa ndoa tu ni pingamizi tosha.

Mkuu Amavubi, kifungu cha 160 cha Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971, kinatoa nafasi kwa mwanamke aliyekaa na mwanaume kwa miaka miwili au zaidi kama mke na mume kupata chochote kutoka katika machumo iwapo mahusiano yao yatavunjika kutokana na kuhitilafiana. Hatahivyo, kifungu hiki hakitengenezi pingamizi kaika kufunga ndoa kama anavyotaka kufanya Mkuu Emmado.

Kwa ufafanuzi huu, Mkuu Emmado, waweza kuoa na huyu binti uliyezaa naye hawezi kuweka pingamizi la kisheria iwapo tu hukuwahi kufunga naye ndoa ya mke mmoja. Mwisho mwishoni, nitumie haki yangu ya ada ya ushauri kabla sijaweka pingamizi ha ha ha ha ha ha ha ha haaaaaaaaaaaaaaaa enjoy Mkuu!
 
Wakuu nameless girl na IDUNDA,mko sahihi. Pingamizi la kihalali kuhusu kufungwa kwa ndoa ni kuwepo kwa ndoa tu. Lakini,hii inategemea aina ya ndoa ambayo ilishafungwa hapo mwanzo.Kama ni ndoa ya wake wengi,bado mume aweza kuoa tena hata kama mke atapinga.Kwa ndoa ya mke mmoja,uwepo wa ndoa tu ni pingamizi tosha.

Mkuu Amavubi, kifungu cha 160 cha Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971, kinatoa nafasi kwa mwanamke aliyekaa na mwanaume kwa miaka miwili au zaidi kama mke na mume kupata chochote kutoka katika machumo iwapo mahusiano yao yatavunjika kutokana na kuhitilafiana. Hatahivyo, kifungu hiki hakitengenezi pingamizi kaika kufunga ndoa kama anavyotaka kufanya Mkuu Emmado.

Kwa ufafanuzi huu, Mkuu
Emmado, waweza kuoa na huyu binti uliyezaa naye hawezi kuweka pingamizi la kisheria iwapo tu hukuwahi kufunga naye ndoa ya mke mmoja. Mwisho mwishoni, nitumie haki yangu ya ada ya ushauri kabla sijaweka pingamizi ha ha ha ha ha ha ha ha haaaaaaaaaaaaaaaa enjoy Mkuu!


kifungu hiki pia kinagusia presumptions of marriage mkuu
 
Bila kuathiri vifungu vya sheria, wakati mwingine huwa napata taabu kidogo nikikaa chini na kutafakari akili za dada zetu hawa..akili zao huwa zinachange often, anachokiwaza sasa kinaweza kuwa tofauti dakika mbili baadaye!

Sijui kwanini watu wanapendana na sijui pia ni mafungamano gani yanawaweka pamoja ila vyovyote iwavyo kwa ushahidi wa kimazingira huyo binti hawezi kukuwekea pingamizi kwenye ndoa unless other wise uwe umeficha kitu hapa.

Kwa kuwa mlipendana kwa dhati kabla, na kwamba upendo huo ukapelekea kupata mtoto na kwa kuwa kwa ridhaa yake,akiwa na akili timamu aliamua kuondoka bila sababu, hatakiwi arudi kwa excuse yoyote...hili likuongoze siku zote.
 
Labda kuongezea hapo Mselewa alipoishia, umetwambia uliishi na mwanamke huyu kwa miaka miwili na mkajaliwa kupata mtoto, je jamii hapo ulipo ilikuwa inawachukuliaje? Je uko kwa wazazi wake walikuwa wanakutambuaje? Walikuwa wanakuchulia kama mkwe wao na uliwahi kujitambulisha na kutoa chochote traditionally ambacho kitatambuliwa kama kutimiza mila katika ndoa? Kama uliwahi kufanya lolote liwe dogo tu ni ushaidi jamii ilikutambua kama mme uliyeoa huyo binti japo mahakama ndiyo itakuwa na uwezo wa kutoa tafsiri kamili
Kwa hiyo tu kama vigezo hapo juu kimojawapo ulifanya jiandae kamili. Kama alivyosema Petro na mimi nikatie kidogo kwa ushauri!! Ahaaaa!!

Wakuu nameless girl na IDUNDA,mko sahihi. Pingamizi la kihalali kuhusu kufungwa kwa ndoa ni kuwepo kwa ndoa tu. Lakini,hii inategemea aina ya ndoa ambayo ilishafungwa hapo mwanzo.Kama ni ndoa ya wake wengi,bado mume aweza kuoa tena hata kama mke atapinga.Kwa ndoa ya mke mmoja,uwepo wa ndoa tu ni pingamizi tosha.

Mkuu Amavubi, kifungu cha 160 cha Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971, kinatoa nafasi kwa mwanamke aliyekaa na mwanaume kwa miaka miwili au zaidi kama mke na mume kupata chochote kutoka katika machumo iwapo mahusiano yao yatavunjika kutokana na kuhitilafiana. Hatahivyo, kifungu hiki hakitengenezi pingamizi kaika kufunga ndoa kama anavyotaka kufanya Mkuu Emmado.

Kwa ufafanuzi huu, Mkuu Emmado, waweza kuoa na huyu binti uliyezaa naye hawezi kuweka pingamizi la kisheria iwapo tu hukuwahi kufunga naye ndoa ya mke mmoja. Mwisho mwishoni, nitumie haki yangu ya ada ya ushauri kabla sijaweka pingamizi ha ha ha ha ha ha ha ha haaaaaaaaaaaaaaaa enjoy Mkuu!
 
Back
Top Bottom