Msaada wa kisheria kuhusu talaka

Mama Joe

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2009
Posts
1,504
Reaction score
840
Jamani wana JF, ninaomba mumsaidie huyu mama msaada wa kisheria jinsi gani apate talaka yake,
" Niliolewa ndoa ya kanisani 1999, nikazaa mtoto mwaka huo huo, tabia ya uzinzi ya mume wangu nikimfumania zaidi ya mara 3 na anakiri na kuomba msamaha, ugomvi, manyanyaso vilinifanya mwaka 2003 kurudi kanisani RC kuomba msaada. Wao walinielekeza nitafute ndugu zake wamwonye, hakusikia, hivyo 2003 nilirudi nyumbani na mtoto kuelezea tatizo. Wazazi walimwita ili aje asikie malalamiko yangu hakutaka kutokea na baada ya miezi 2 waliniambia nikachukue changu niondoke hapo, hakujali alisema niende tu hana shida na mimi. Hivyo miaka yote hii ninalea mtoto na nimekaa mwenyewe. Karibuni nimeona napoteza muda na ningependa kuolewa tena, kanisani wameniruhusu, ila nikavunje hiyo ndoa mahakamani.
Tatizo nimeanzia ustawi wa jamii wananiambia nimlete huyu mume hapo wakati mie sijui hata sasa hivi anaishi wapi, bahati nzuri karibuni nikaitwa na wenzie nikamuone amelazwa mgonjwa sana hospital, ila alipotoka tu sijui tena alipo. Sasa mie ombi langu ni nipate talaka yangu, je inawezekana niende mahakamani moja kwa moja na kudai bila hawa ustawi wanaonizungusha?
Pili kutokana na hali yake nadhani hataweza kusimama mahakamani, nami wala sintapenda kumsimamisha mgonjwa namuonea huruma je mahakama inaweza toa talaka hata kama mwingine hajulikani aliko?"
Mie sio mwanasheria msaada wenu please nimjibu nini, asante
 
Mama Joe..
Asante kwa kisa hiki.
Kwa kawaida mwanandoa yeyote anayedai talaka ana jukumu la kuthibitisha kwamba ndoa imevunjika kabisa (marriage has broken down irreperably), hii ndio test ya kwanza kabisa ambayo huyu mama atatakiwa kuthibitisha.,sasa ataweza vipi kufanya hivyo, ni kupitia ushahidi wa matukio kama hayo ya uasherati (adultery).
Kwa msaada zaidi nakuwekea vifungu hivi vya Sheria ya Ndoa ya Tanzania Sura ya 29 [RE:2002]

Hiki ni kifungu cha 99

Hiki ni cha 107(2)

Lakini sheria inataka kwamba kabla hujapeleka maombi ya talaka mahakamani ni lazima kwanza upite katika baraza la usuluhishi la ndoa ambalo lina jukumu la kuwapatanisha na ikishindikana wao wanacertify kuwa wameshindwa kuwasuluhisha hivyo muende mahakamani, sasa kwa case ya huyu mama ambaye hajui mumewe yupo wapi basi sheria inampa uwezo wa kutokwenda kwenye baraza la usuluhishi hivyo kwenda mahakamani moja kwa moja, kifungu hiki cha 101 (a) Kinahusika zaidi.

ANGALIZO
Kifungu hiki cha sheria kitamsaidia iwapo tu atabadili sababu ya maombi yake ya talaka kutoka kwenye uasherati (adultery) na kuwa kutelekezwa (dessertion) ili kumsaidia kupata talaka yake haraka kwani inavyoonekana kutokomea kwa huyo mume mi mpango wa makusudi ili huyu mama asifanikiwe lengo lake.
 
Mahakama haiwezi toa talaka hadi pande zote zisikilizwe na uthibitisho uwepo kwamba alitenda kosa ulilolitaja.Yamkini yeye aweza kusema anakupenda na hana mpango wa kukuacha na hatoi talaka.Hiyo inakuwa vigumu ila kama kuna uthibitisho wa yeye kufumaniwa,au ushahidi wa jinsi asivyoweza kukuhudumia basi kwa hali hiyo mahakama itatumia busara kuweza kusaidia kupata talaka.Lakini Mama Joe kama umesema hali yake ni mahututi yamkini Israeli atamtembelea wakati wowote basi na iwe amri ya Mungu pale kifo kitakapowatenganisha.
 

Naona hapa ndio anapokwama maana miaka imepita, na huo ushahidi wa kitu gani ampeleke mashahidi au nini, maana ni kama ameamka toka miaka mingi aliyoachwa na kutaka haki yake, sijui napo kakosea?
 
mama joe,asante kwa kisa hiki but my advice iz huyo mama kapima lkn?maana isije ikawa anataka ndoa but pia hajajua kuhusu afya yake.ZINGUKA,TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA
 
Hii pia ni option nyingine, ila mtu ukae unamuombea mbaya wako afe ili wewe uolewe naona ni issue nyingine, ndio maana kanis ala huyu mama limempa uhuru ila tu hiyo ndoa yake ivunjwe isilete mushkeri.
Sasa mie najiuliza huyu mtu ambaye miaka saba haonekani kisheria anatambulika ni mume? Namaanisha kitu gani aonyeshe kuwa huyu mtu sijui alipo wala matunzo kwa mtoto sipati?
 
mama joe,asante kwa kisa hiki but my advice iz huyo mama kapima lkn?maana isije ikawa anataka ndoa but pia hajajua kuhusu afya yake.ZINGUKA,TANZANIA BILA UKIMWI INAWEZEKANA

Thanks dear, ni mzima wa afya na ni best wangu tulimshauri kupima mara tu alipoondoka kwa mumewe, pia mwaka jana amepima, hana tatizo kabisa.
 
ok thats very gud dia,pole kwa matatizo haya ndo todays news kila sikuni talaka kuachana thats our planet Earth
Thanks dear, ni mzima wa afya na ni best wangu tulimshauri kupima mara tu alipoondoka kwa mumewe, pia mwaka jana amepima, hana tatizo kabisa.
 

Hapa nimekusoma nami nakubaliana nawe nahisi mwanamme anafanya kusudi, naona arudi tena barazani na kuwaeleza hili kwa mara nyingine, kisha aende tu mahakamani kujaribu tena
 
ok thats very gud dia,pole kwa matatizo haya ndo todays news kila sikuni talaka kuachana thats our planet Earth
Ni kweli yaani inasikitisha watu kufanya life commitment halafu wasizitimize, wanachukulia simple tu, mbaya zaidi mtoto anakosa malezi ya mzazi mmoja
 
Sambamba na michango mingine, hoja iliwahi kujadiliwa hapa hivi:

 
Ustawi wa Jamii bongo ni longalonga tu. Hawa ndio wanaowafanya wanawake wengi hata wanaume wanateseka kupata haki zao. Talaka ni haki ya mdai na mdaiwa kwa nini iwe na uwalakini. Wenyewe wameshafika mahali hawawezani tena ninyi mnataka wasuluhishe ili iweje? Ombi la talaka linachukua miaka kumi huku si kunyimana haki wajameni? Mahakama, Ustawi wa jamii wote dugu moja rushwa kwa sana ndio tatizo.
 
Jamani nashukuru sana kwa msaada huu, maana binafsi nimekaa na swali hili muda sikuwa najua nimsaidieje, mbarikiwe wote. Na print hizi inforamtion zoote nadhani wiki ijayo ataanza tena kudai haki yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…