katika criminal case, kama kesi imefunguliwa mahakama kuanzia ya wilaya kwenda juu, hauwezi kumwona mlalamikaji akaja pale ikiwa na maana ya victim wa ile crime, bali mlalamikaji wake huwa ni jamhuri(ikiwakilishwa na wakili wa serikali au public prosecutor mwenye mamlaka aliyopewa na dpp). hivyo, katika kesi yako kama iko mahakama ya wilaya, mlalamikaji ni huyo mwendesha mashitaka, victim atakuja tu kama shahidi. makosa ya jinai yaani yale ambayo raia anafanya jinai dhidi ya raia mwingine, kwasababu katiba ya nchi inaipa serikali wajibu wa kuwalinda watz wote, basi ukimfanyia jinai raia serikali inao wajibu kumlinda, yaani kukushitaki badala yake yeye, hivyo jinai dhidi ya raia ni jinai dhidi ya serikali na wakili wa serikali/public prosecutor atakushitaki (wakimuwakilisha dpp). mawakili wa serikali wapo kila mkoa kwa sasa, uliza katika kila makao makuu ya mkoa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali ipo wapi, watakuonyesha, ukienda polisi kuuliza hao lazima watakuonyesha kwasababu sik,u hizi polisi wakikamata mtu hawaandai hati ya mashitaka lazima wapeleke jalada ofisi ya mwanasheria mkuu wakaandae na kupeleka mahakamani, polisi wanapeleka mahakamani watuhumiwa tu (katika maeneo yale ambayo ofisi ya mwanasheria mkuu imefunguliwa).
wakati mwingine, hatujui ni kosa gani ndugu yako anashitakiwa nalo, ungetuambia tungejua na kukushauri, lakini maadamu ni bailable(umesema polisi wanataka rushwa), naamini ukitimiza vigezo ataweza kupata dhamana. polisi hawana mamlaka kutoa dhamana kwa mtu pale ambapo atakuwa ameshafikishwa mahakamani, limit ya uwezo wao kutoa dhamana ni pale tu ambapo suspect amekamatwa tu hajafikishwa mahakamani bado, akifikishwa mahakamani tu ndani ya masaa 24 (au zaidi kama kuna sababu maalumu), mamlaka yote haiko kwao tena, bali mahakama ndiyo yenye mamlaka kutoa dhamana au la, na huweka conditions ambazo wakili wa serikali/mwendesha mashitaka pia anaweza kupinga kama ataona mahakama inaenda kinyume na sheria, ila mahakama ndiyo yenye mamlaka.
wakati mwingine kesi inaweza kuchukua mda mrefu kwasababu ya nature ya upelelezi. ukitoa hizo hela polisi watakulia hela bure na hawawezi kukusaidia. wanaweza kukudanganya kuwa izo hela utakazotoa wataenda kuwahonga mahakmimu etc, lakini niwajuavyo polisi watazila na hutafanikiwa. tuambie kosa alilotenda, ipo mahakama gani, na amepewa conditions gani za bail/dhamana ili tukushauri vizuri. hapa ndani kuna mawakili wa serikali wengi tu, utapata majibu.