Kingcobra
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 1,000
- 310
Wataalam wa sheria,
Salaam kwenu na poleni na majukumu ya kila siku.
Kuna Dada yangu mmoja mume wake alifariki akiwa njiani kutoka kazini kuerejea nyumbani. Ilikuwa ni mida ya jioni alipokutana uso kwa uso na lori yeye akiwa anaendesha pikipiki. Waligongana kwa kosa la mwenye lori na akafariki hapo hapo. Nimesema kwa kosa la dereva wa lori kwa sababu ndiyo rule ya mahakama na dereva wa lori alikiri hivyo.
Baada ya msiba, mwajiri wa mume wa dada yangu aligharamia sanda, jeneza, shada la maua na usafiri wa magari mawili kwa ajili ya kusafirisha kwenda kwenye mazishi ndugu wa marehemu pamoja na mjane. Pia, mwajiri alitoa rambirambi kama taasisi na michango kutoka kwa wafanyakazi na kutoka kwa makampuni yenye mahusiano na taasisi aliyokuwa anafanyia mume wa dada yangu.
Sasa nachotaka kujua ni je, sheria inasemaje kuhusu fidia ya mwajiri kwa mjane maana marehemu shemeji yangu ameacha familia ikiwa na watoto wanaohitaji matunzo na kusoneshwa. Je, alichotoa mwajiri kinatosha au kuna kingine zaidi ikizingatiwa kuwa marehemu alipata ajali akiwa ametoka kazini kuelekea nyumbani?
Tafadhali wajuzi wa sheria wanisaidie katika hilo ili nami nione ni namna gani tunaweza kumbana mwajiri.
Salaam kwenu na poleni na majukumu ya kila siku.
Kuna Dada yangu mmoja mume wake alifariki akiwa njiani kutoka kazini kuerejea nyumbani. Ilikuwa ni mida ya jioni alipokutana uso kwa uso na lori yeye akiwa anaendesha pikipiki. Waligongana kwa kosa la mwenye lori na akafariki hapo hapo. Nimesema kwa kosa la dereva wa lori kwa sababu ndiyo rule ya mahakama na dereva wa lori alikiri hivyo.
Baada ya msiba, mwajiri wa mume wa dada yangu aligharamia sanda, jeneza, shada la maua na usafiri wa magari mawili kwa ajili ya kusafirisha kwenda kwenye mazishi ndugu wa marehemu pamoja na mjane. Pia, mwajiri alitoa rambirambi kama taasisi na michango kutoka kwa wafanyakazi na kutoka kwa makampuni yenye mahusiano na taasisi aliyokuwa anafanyia mume wa dada yangu.
Sasa nachotaka kujua ni je, sheria inasemaje kuhusu fidia ya mwajiri kwa mjane maana marehemu shemeji yangu ameacha familia ikiwa na watoto wanaohitaji matunzo na kusoneshwa. Je, alichotoa mwajiri kinatosha au kuna kingine zaidi ikizingatiwa kuwa marehemu alipata ajali akiwa ametoka kazini kuelekea nyumbani?
Tafadhali wajuzi wa sheria wanisaidie katika hilo ili nami nione ni namna gani tunaweza kumbana mwajiri.