Msaada wa kisheria: Nimeibiwa pesa yangu kwenye line yangu ya vodacom

Msaada wa kisheria: Nimeibiwa pesa yangu kwenye line yangu ya vodacom

Kalunguine

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2010
Posts
2,543
Reaction score
134
Mimi ni mtanzania mjasiriamali,katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita nilikuwa na kiasi cha pesa za kutosha katika akaunt yangu ya M-PAWA,nilipokuwa nikijaribu kutoa pesa kutoka mpawa kuja mpesa nikawa napata ujumbe wa kuwa sijafaulu kutoa pesa nilizokuwa nataka kutoa.

katika kipindi chote hicho nimekuwa nikipiga simu huduma kwa wateja mara kwa mara kuomba utatuzi wa shida yangu bila mafanikio.

jambo hili kwa kiasi fulani limenirudish NYUMA kiuchumi kwani pesa hizo zilikuwa ni za kununulia bidhaa ambazo kwa namna moja ama nyingine zingekuwa zimeniingizia faida ya takriban ya shilingi milioni 4.5 kwa kipindi chote hiki ambacho pesa zangu zimezuiwa kutoka katika line yangu.

jambo baya zaidi na la kushtua katika kipindi cha wiki moja nyuma kutoka sasa kila napoangalia salio langu la mpawa naambiwa salio langu ni tsh 0!

OMBI LANGU: sheria zinasemaje kwa mambo kama haya?

sheria mpya ya makosa ya mtandao inanilindaje ili nipate haki yangu?

#Vodacom
 
Nenda HQ pale mcity kitengo cha M pesa utapata majibu ucporidhika ndio uende tcra
 
Kwanza kabisa, pole kwa shida hiyoiliyokuletea usumbufu kifedha na kifikra. Kwa faida yako ya baadaye naomba zingatia haya yafuatayo wakati unashughulikia swala lako:

1. Ni vema ubadili kabisa taarifa zako za Mpesa; badili ph# yako, futa namba yako ya siri ya utambulisho- Personal Identification Number (PIN),
2. Jizoeze kutoweka kiasi kikubwa cha pesa Mpesa hasa kuanzia milioni kadhaa,na kama unaweka basi iwe ni kwa kuzipishia kwa muda tu kwa lengo la kuzipeleka kwenye hitaji husika. Mind you,system mara zote itaonyesha Mpesa Accts ambazo mara nyingi zina hela nzuri (pesa ndefu),na hii inakuwa accessed na wahudumu/staff wa mtandao husika - sasa hapa usalama wa pesa ya mteja inategemea sana usiri na uadilifu (confidentiality and integrity) wa hao staff. Sisemi kwamba wao sio waaminifu, nina maana kwamba wasipokuwa makini hata kama n kwa nia njema, taarifa za mteja zaweza kuwafikia watu wengine wasio wema, na hivyo kupelekea mteja kupata usumbufu kama huo.
3. Uwe makini sana na mawasiliano ya kifedha kwenye mtandao (online transactions) kwani huku kwetu hasa 3rd world countries,bado hatujawa na uadilifu wa kutosha kuhusiana na usalama wa taarifa zetu, na zaidi sana hatujawa na uwezo wa kutosha kukabiliana na uhalifu wa kimtandao.
4. Jitahidi kuwasiliana na kampuni husika kwa swala la "Vigezo na Masharti Kuzingatiwa". Jitahidi ufahamu hivyo vigezo vyote na masharti ya kuzingatiwa, na upate kimaandishi. Mind you, makampuni na taasisi nyingi in 3rd world TZ tukiwamo, huendesha biashara kwa misingi ya "Ujinga" wa wateja wao,hivyo kupata faida "nono"zilizopitiliza kwa sababu mteja akipata tatizo hajui/haelewi na hawezi kufuatilia haki zake. Waliolala tuamke.

Naomba kuwasilisha
 
Back
Top Bottom