Msaada wa Kisheria tafadhali

Msaada wa Kisheria tafadhali

Baba Collins

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2011
Posts
502
Reaction score
106
Heshima zenu wakuu,

Naomba kujuzwa ni haki zipi anapata mtu anyeachishwa kazi kutokana na sababu za kiutendaji za kampuni?
 
Heshima zenu wakuu,

Naomba kujuzwa ni haki zipi anapata mtu anyeachishwa kazi kutokana na sababu za kiutendaji za kampuni?
kujibu hili swali inabidi mtu afanye scenerio nyingi na kuona ni haki gani unaweza kupata. Funguka kidogo, sababu za kiutendaji kama zipi: kampuni inapata hasara na kutaka kufunga biashara au kampuni haiwatendei haki watumishi?
 
kujibu hili swali inabidi mtu afanye scenerio nyingi na kuona ni haki gani unaweza kupata. Funguka kidogo, sababu za kiutendaji kama zipi: kampuni inapata hasara na kutaka kufunga biashara au kampuni haiwatendei haki watumishi?

Nakushukuru Mh.Kimbunga. Kwa ufupi kampuni iko katika mdororo wa kiuchumi na hivyo ina mpango wa kunguza wafanyakazi (Retrenchment). Je,ni haki zipi mtu anayepunguzwa anastahili kuzipata hususan malipo yake?
 
Kama kampuni imekumbwa na mdororo wa kiuchumi na imethibitika hivyo, kwa mujibu wa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2004, kifungu cha 44, Mwajiri atapaswa kumlipa Mfanyakazi stahiki zifuatazo.
1. Ujira wowote wa siku alizofanya kazi kabla hajaachishwa kazi.
2. Malipo yoyote ya likizo ya mwaka na kama kuna malimbikizo ya likizo ambazo hakwenda.
3. Malipo ya notisi, ambayo ni mshahara wa mwezi mmoja.
4. Malipo ya kiinua mgongo, ambayo kiwango cha chini kabisa ni malipo ya mshahara wa siku 7, zidisha miaka uliyofanya kazi isiyozidi 10
5. Posho ya usafiri wako wewe mwenyewe na familia yako, pamoja na nauli ya mizigo, hadi mahali alipokuajiri Mwajiri wako.
 
Kama kampuni imekumbwa na mdororo wa kiuchumi na imethibitika hivyo, kwa mujibu wa Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2004, kifungu cha 44, Mwajiri atapaswa kumlipa Mfanyakazi stahiki zifuatazo.
1. Ujira wowote wa siku alizofanya kazi kabla hajaachishwa kazi.
2. Malipo yoyote ya likizo ya mwaka na kama kuna malimbikizo ya likizo ambazo hakwenda.
3. Malipo ya notisi, ambayo ni mshahara wa mwezi mmoja.
4. Malipo ya kiinua mgongo, ambayo kiwango cha chini kabisa ni malipo ya mshahara wa siku 7, zidisha miaka uliyofanya kazi isiyozidi 10
5. Posho ya usafiri wako wewe mwenyewe na familia yako, pamoja na nauli ya mizigo, hadi mahali alipokuajiri Mwajiri wako.


Nashukuru sana mkuu nimekusoma vyema kabisa!
 
Back
Top Bottom