Msaada wa kisheria

Mchelle

Member
Joined
Mar 20, 2010
Posts
95
Reaction score
28
Nawasalimu wana jamvi,
naomba yeyote anayejua kuhusu sheria zetu hapa nchini

mimi nilikuwa nafanya biahara na jamaa fulni hlafu tukaja kukosana kabisa. Tukakubaliana kulipana ili mimi nimlipe yeye aniachie aondoke. Baada ya kumlipa zaidi ya 60% tulikubaliana nimalizie balance kwa muda wa miezi mitatu. Yule jamaa kwa wivu mbaya akaenda kuingilia biashara yangu kwa mambo mengi sana kuiharibu. Baada ya hapo ilibidi nishindwe nikaacha ile biashara kabisa. Yule jamaa kwa kuwa nilimwahidi kumlipa akaenda police kunishtaki kwa kosa la jinai. Police wakaja kuniona wakinitaka niende kituoni nikajibu shtaka.

Nawaombeeni msaada kisharia hapo!
 
Issue yako ipo too complicated. Ina mambo mengi ambayo wewe umeyafungia kwenye point moja tu. Labda tuanzie hapa,
1. Makubaliano yenu ya biashara mwanzo yalikuwa ya maandishi? na mlikubaliana nini hasa?
2. Nini hasa chanzo cha ugomvi wenu kibiashara?
3. Makubaliano yenu ya kulipana baada ya ugomvi yalikuwa ya maandishi?
4. Ugomvi alioleta mwenzako katika biashara yako, chanzo hasa kilikua nini?
5. Katika ugomvi huo, mwenzako alisababisha vipi wewe kukwama?
 
acha kueleza vitu kifupi sisi hatukuwepo katika ugonvi wenu eleza vitu vyote vya msingi tujue jinsi ya kukusaidia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…