Tafadhari, kama kichwa kinavyosema.
Nina kitabulisho cha taifa nilijiandikishia Dar ila kwa sasa nipo mkoani. Lakini nilipochukua niliangalia picha na majina juu juu na kuweka sahihi na kuondoka kwa sababu ya kuchoka kufuatilia na foleni. Lakini baadae nikagundua kwamba kuna herufi imekosewa katka jina la katikati.
Sasa naombeni kujuzwa. Je, naweza kurudi Dar kukirekebisha au nikarekebishia mkoani? Na je, muda wa marekebisho unaweza kuwa kama kusubiri kitambulisho kipya? Na je, nitahitajika kubeba documents zote? Msaada tafadhari.
Nitashukuru kwa msaada wenu.