Msaada wa mawazo: Mzunguko huu watuchanganganya

Msaada wa mawazo: Mzunguko huu watuchanganganya

Prince Nadheem

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2012
Posts
1,259
Reaction score
1,056
Habari za maandalizi ya Eid wadau wa JF Doctor? straight to the point, mie na mke wangu tunatumia njia ya uzazi wa mpango ya kalenda. Sasa safari hii hajaziona siku zake yapata mwezi sasa, tumeshacheki mimba mara tatu hadi nirushapo uzi huu ila majibu mara zote ni negative. hali hii inatupa hofu sana as hatujui nini kinaendelea. Tafadhali ushauri ila kama wajiona wataka kuleta mzaha na kebehi pita wima.
Cc: @mzizimkavu
 
Huyo mkeo hajasafiri wala kupata tatizo lolote la kiafya?
 
Habari za maandalizi ya Eid wadau wa JF Doctor? straight to the point, mie na mke wangu tunatumia njia ya uzazi wa mpango ya kalenda. Sasa safari hii hajaziona siku zake yapata mwezi sasa, tumeshacheki mimba mara tatu hadi nirushapo uzi huu ila majibu mara zote ni negative. hali hii inatupa hofu sana as hatujui nini kinaendelea. Tafadhali ushauri ila kama wajiona wataka kuleta mzaha na kebehi pita wima.
Cc: @mzizimkavu

Hana gubu?
 
Naona ni mapema sana kutaka kujua.

Vuta subira maan sio mchepuko ni mkeo.

By th way kalenda sio reliable sana kwa uzazi wa mpango.
 
mkuu shaka ya nini mbona mwezi kitu kidogo sana.
ingekuwa labda ka kaa miezi mi 3 hapo sawa tungesema kuna tatizo.lakini kwa huo mwezi bado mapema sana kushikwa na wasi wasi vuta subila kidogo.
 
Halafu sijui wife nae kaingiwa na hofu psychologically, maana jana na leo analalama kuwa tumbo kama linavuruga. Sasa sijui hapo shida itakuwa nini?? Ushauri zaidi tafadhali.
 
tumbo likisumbua sana amwone daktari wajue kunani huko tumboni... usiridhike na hiyo hali, mwanamke kukosa hedhi na mimba hana si jambo la kawaida. subiri huu mzunguko wake uishe ukipita kavu basi muwahishe hospitali.
 
Back
Top Bottom