Msaada wa tatizo la kuvimba tumbo

Hornet

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2013
Posts
26,486
Reaction score
51,156
Habari zenu jamani.

Kuna jamaa yangu nimepita kumsalimu ila hali yake si shwari kabisa.
Amevimba tumbo anasema ni mwezi wa sita sasa, anasema tumbo linauma
amepoteza hamu ya kula na hata akila anakula kidogo sana.

Naombeni msaada wenu nijue nianzie wapi kumtafutia tiba ya ugonjwa huu.
Je unafahamika kitaalamu?

Kwa Dar es salaam ama Mbeya ni wapi naweza kumpatia matibabu?
Binafsi nilifikiria kumpeleka Muhimbili.

Tumbo lina ukubwa kama ujauzito wa miezi saba-nane.
 
mpe pole sana mkuu..ngoja wajuz waje naimani atapata msaada..
 
Ni Muhimbili tu. Ameharibu inni kwa kunywa pombe nyingi. Kwa hiyo chakula hakisagigi. Wahi Muhimbili
 
Kaka huyu atakuwa na tatizo kwenye INI
Kitaaalam linajulikana kama Liver cirrhosis
Anaweza anza tapika damu , na kuvimba miguu pia
PM me tuongee zaidi
 
"Kuna ndugu yangu aliumwaga ugonjwa kama huo miaka mingi kidogo, ila ishu ni uparesheni hapo utumbo utakuwa umeongezeka urefu wa kipimo kinachotakiwa kwa mwanadamu na badala yake hawezi kupata hamu ya kula na hata akila basi ni kidogo sana na anaweza kukaa siku tatu bila kwenda choo kwasabab utumbo unasafirisha taka unakuwa una tatizo na kupunguza perfomance yake. kupona atapona iwapo mwenyez mungu atapenda ndugu yetu aishi. nenda naye hospitali wapige x-ray... kila la kheri mkuu mungu awe pamoja nanyi"
 
ahsante sana jumatatu ntafanya hivyo. chakula anakula kidogo mno yaani toka jana mchana mpaka leo hajala chochote.
 

Mi siyo daktari ila nahisi ni tatizo la ini. Mpe Lactulose ambayo unaweza pata pharmacy bila cheti ina majina kama osmolax anywe hata 30 mils uone kama hatapata choo. Hii ni tempo msaada ila wasikilize madaktari.
 
kuharibika ini siyo mpaka pombe. kuna hepatitis pia.
 
Tumbo lina mambo mengi. Kama unasema hajawahi kutibiwa, ni lazima aonane na tabibu ili upembuzi yakinifu ufanywe. Usijaribu kufanya matibabu kiholela bila ya kupata ushauri wa kitaalam. Inasikitisha kuona watu humu ndani wanatoa ushauri kwa kukisia tu bila ya kupata maelezo ya kutosha, kufanya vipimo na kujua ni nini hasa tatizo la mtu. Kama ni kweli hajawahi kupata matibabu, basi aanzie hapo.
 


Umefanikiwa kupata matibabu!?
 
Umefanikiwa kupata matibabu!?
ndiyo mgonjwa nipo naye nyumbani anaendelea kutumia dawa, maji yameondolewa na wanasema ni tatizo la ini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…