Msaada wa tiba au ushauri mniokoe jamani!!!!

ufumawicha

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2014
Posts
504
Reaction score
209
Ni mwaka wa 18 sasa nasumbuliwa na tumbo linajaa gesi na kuunguruma sana hadi naogopa kukaa na wenzangu. Cha ajabu pia hata mwili ukipata joto kiasi cha kutoa jasho nahisi kuchomwachomwa mwili mzima mithili ya mtu aliyeng'atwa na siafu.

Nimezunguka hospitali nyingi hadi Muhimbili lakini naambiwa sina tatizo,sijui nifanyeje.Baada ya Muhimbili nilienda hapo kwa hao watu wa NATURAL THERAPIES CENTER nao wakala hela zao lakini wapi.

Ushauri please!
 
  • Kuna uwezekano una lactose intolerance,una mapungufu au huna enzyme inayoitwa lactase inayotegenezwa na bakteria(lactic acid bacterias) kwenye tumbo ambao wanavunja vunja lactose(ni sukari inayopatikana kwenye maziwa na products za maziwa kama siagi,mtindi,cream n.k),kwahio inasababisha tumbo kujaa gesi,kunguruma,kuuma,kuhara na hata kujamba sana.Tiba ni kula vidonge vyenye hizo enzyme haswa unapokula vyakula vyenye lactose.Au kutumia maziwa na product za maziwa ambazo ni lactose free.Ukitaka kujua kama ni maziwa au product zake zinasababisha hali hio epuka kuyatumia kwa muda wa wiki mbili uchunguze kama tumbo linaendelea kunguruma.
  • Tiba nyingine ni kula vidonge vyenye hao lactic acid bacterias kama replacement.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…